• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

NAWAPONGEZA KWA UJENZI WA ZAHANATI 'DC MACHALI'

Imewekwa kwenye: December 7th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Moses Machali amewapongeza wananchi  wa Kijiji cha Tumuli, Kata ya Tumuli kwa uamuzi wao wakuanza ujenzi wa zahanati katika kijiji hicho na kuwataka  kuendelea na juhudi hizo  hadi kukamilisha ujenzi huo ili kusogeza huduma karibu kuepusha changamoto ya kufuata huduma za afya katika kijiji cha Maluga kilichopo Wilaya ya Iramba na kijiji cha Iguguno .

Ameyasema hayo Disemba 06, 2023 katika muendelezo wa ziara zake za kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika kijiji cha Tumuli, Kata ya Tumuli Wilayani Mkalama.

‘’Niwapongeze wananchi wa Tumuli kwa uamuzi wenu wa kuanzisha ujenzi  wa zahanati hii mmefanya uamuzi mzuri sana niwapongeze sana , niwaambieni tu maendeleo hayaletwi na serikali pekee’’ Alisisitiza Mhe. Machali.

Amewasisitiza kuharakisha kukamilisha ujenzi huo ili serikali iweze kuwaletea wataalamu pamoja na vifaa tiba katika kusogeza huduma karibu na kuwaondolea adha ya kufuata huduma mbali.

Aidha Mhe. Machali aliwataka kuwashirikisha wataalamu wa majengo kukagua na kuthibiti viwango na ubora wa jengo hilo na kuepuka makosa  na hasara iliojitokeza katika jengo la awali ambalo lilikuwa hatua ya ukamilishaji na kuonekana halina ubora .

‘’Nitawaletea msanifu majengo ‘Quantity Surveyor’ kuja kulikagua jengo hili ili kuepusha makossa yaliyojitokeza hapo awali katika jengo la zahanati ambalo lilibainika halina ubora na halifai kwa matumizi’’ aliongeza Mhe. Machali.

Ameendelea kuwasisitiza wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali kuchangia maendeleo mbalimbali huku akiwataka kuendelea kuwapa ushirikiano watendaji na wataalamu ambao serikali imewaamini kwaajili ya kuwatumikia ambapo amesema mwananchi asiyechangia maendeleo yao hafai kutembea pamoja katika safari ya mafanikio.

Katika hatua nyingine Mhe. Machali ameongeza kuwa serikali inahakikisha inatatua changamoto katika sekta mbalimbali ikiwepo Afya, Kilimo,mifugo na uvuvi, Elimu, Maji , barabara ndio maana amekuwa na utaratibu wa kutembea kila kijiji kwaajili ya kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.