• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Nane nane ionekane huko kwa wananchi wenu- Nchimbi

Imewekwa kwenye: August 4th, 2018

‘’Nyie wote mlioshiriki katika maadhimisho haya ya Sikukuu ya Wakulima na wafugaji mnatakiwa kuhakikisha yale mliyojifunza yanaonekana kupitia kwa wananchi wenu huko mlipotoka’’

Ni moja ya kauli zilizotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Daktari Rehema Nchimbi wakati wa hotuba yake muda mfupi kabla hajafungua rasmi maadhimisho ya 22 ya Sikukuu ya Wakulima na Wafugaji kanda ya kati maarufu kama Nane nane yanayoendelea hapa jijini Dodoma.

Katika hotuba yake Mhe. Nchimbi alibainisha kuwa mwaka huu wa fedha Serikali imetenga shilingi trilioni 13.8 kwa ajili ya Kilimo na Mifugo hivyo aliwataka wadau wa sekta hizo kutumia fursa hiyo vizuri na kuhakikisha sekta za kilimo na mifugo zinakuwa chachu ya kuhakikisha azma ya Tanzania kuelekea kwenye uchumi wa viwanda inatimia.

“Leo wakati natembea kwenye mabanda mbalimbali nimekutana na mkulima ambaye katika maelezo yake amenieleza kupitia boga moja nililomkuta nalo badala ya kuliuza shilingi elfu 10 ana uwezo wa kulitumia  kuingiza zaidi ya shilingi laki moja kwa kutengeneza juice, maandazi na keki” Alisema Mhe. Nchimbi.

Mhe. Nchimbi alisema kuwa hivi sasa zao la korosho  limekuwa ni zao mkakati katika mikoa ya Dodoma na Singida  ambapo viongozi wa mikoa hiyo wanataka kuhakikisha ndani ya miaka minne ijayo mikoa hiyo itakuwa vinara wa mazao hayo.

“Kwa bahati mbaya katika maeneo yaliyozoeleka kulima mazao hayo tafiti zinaonesha wanavuna mazao hayo mara moja tu kwa msimu lakini huku kwetu hasa mkoani Singida imeshathibitika zao la korosho kuweza kuvunwa mara mbili kwa mwaka” Aliongezea Mhe. Nchimbi.

Mhe. Nchimbi amewataka Wakulima kujikita kwenye kilimo cha umwagiliaji ili kuendelea kuongeza kipato kupitia sekta hiyo kwa mwaka mzima badala ya hivi sasa ambapo wakulima wengi baada ya kuuza mavuno yao hushinda vijiweni huku wakisubiri msimu wa masika.

Nimekuwekea video fupi ya sehemu ya hotuba ya Mhe. Nchimbi akizungumza leo muda mfupi kabla hajafungua rasmi maadhimisho hayo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.