• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

NAIBU KATIBU MKUU MAZINGIRA AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MKALAMA

Imewekwa kwenye: May 17th, 2023

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dr. Sweetbert Zakaria Mkama ametembelea na kukagua miradi inayotekelezwa kupitia Mradi wa kurejesha Ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame Wilayani Mkalama kwa Vijiji vya  Munguli, Nyahaa,pamoja na Lugongo ambapo ametaka kuongeza usimamizi katika miradi hiyo ambayo inaonekana kusua sua kukamilika.

Akiongea  katika ziara hiyo Mei 17 2023  Dr. Mkama amesema serikali inatoa fedha nyingi kwaajili ya kuharakisha maendeleo kwa wananchi lakini wasimamizi wa Miradi wamekuwa wakikwamisha miradi kukamilika kwa wakati .

‘’Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mama Yetu Dkt. Samia Suluhu Hassani inatoa fedha hizi kwaajili ya kuleta maendeleo kwa wananchi lakini kwanini mnataka kumkwamisha mama?mbona miradi mingine mnakamilisha kwa wakati? Kwanini hii ya mazingira? Fedha zote  anatoa Mama hivyo hakuna miradi ‘Grade A, B wala F’ serikali ikitoa fedha lazima miradi yote ipewe kipaumbele kama ilivyo kwa miradi mingine” Alisisitiza Dr.Mkama.

Dr. Mkama  ametaka thamani ya pesa iendane na  miradi inayotekelezwa pamoja na michoro yote ‘BOQ’ ambapo amewataka kufuata  maelekezo nasio kufanya tofauti na mwongozo unavyosema .

Pamoja na hayo aliwataka wasimamizi wa miradi hiyo kuongeza kasi ya usimamizi ili miradi hiyo ilete tija kwa wananchi ambao wamesubiri kwa shauku kubwa  waweze kujiletea maendeleo pamoja na kukuza uchumi na kuwanasua katika hali ngumu ya maisha.

Miradi iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa Jengo la kuchakata asali katika Kitongiji cha Kipamba Kijiji cha Munguli, Ukarabati wa Josho katika Kijiji cha Nyahaa pamoja na Ujenzi wa Jengo la kuchakata Nafaka katika Kijiji cha Lungongo.

Ziara hii inakuja siku chache baada ya ziara ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Sulemani Jafo kutembelea Wilayani hapa na kukagua miradi ya kurejesha Ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa Chakula katika maeneo kame.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA TATHMINI YA LISHE ROBO YA NNE – WILAYA YA MKALAMA 2025

    September 03, 2025
  • KONGAMANO LA HUDUMA ZA KIFEDHA WILAYANI MKALAMA

    August 19, 2025
  • MWENGE WA UHURU, WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 36 MKALAMA 2025

    July 21, 2025
  • SERIKALI YAKABIDHI KADI ZA MATIBABU BURE KWA WAZEE MKALAMA

    June 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.