• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mwenge wa Uhuru 2017 ulivyokimbizwa Mkalama

Imewekwa kwenye: July 6th, 2017

Siku ya jumatatu ya wiki hii (Julai 3,2017) Wilaya ya Mkalama ilikimbiza Mwenge wa Uhuru baada ya kuupokea kutoka Wilaya ya Iramba ambapo ulikimbizwa katika Miradi 7  iliyopo Wilayani hapa huku  minne ikiwa ni ya kuwekwa jiwe la msingi, miwili ya kuzinduliwa na mmoja wa kukaguliwa/kuonwa.

Miradi hiyo ni pamoja na  wa ujenzi wa bweni kubwa la wanafunzi, bwalo la chakula na vyoo unaoendelea katika shule ya sekondari Iguguno, mradi wa maji safi uliopo katika kijiji cha Mnolo, Mradi wa Kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti na ufugaji wa nyuki uliopo katika kijiji cha Kinyangiri, mradi wa Ujenzi wa Ukumbi mkubwa wa Mikutano na hadhara mbalimbali uliopo katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya katika kijiji cha Nduguti, mradi wa ujenzi wa barabara ya Kijiji cha Mwando mpaka kijiji cha Nkalakala  na mradi wa soko la Vitunguu uliopo katika kijiji cha Dominiki.

Jumla ya gharama ya miradi yote hiyo mpaka kukamilika kwake ni shilingi 5,197,865,111 ambapo michango iliyotolewa kupitia nguvu za wananchi  ni shilingi 35,770,000 huku fedha iliyotolewa na serikali kuu ikiwa ni shilingi 1,694,878,769  Upande wa Halmashauri ya Wilaya imetoa  shilingi  9,580,000 huku wahisani wakitoa shilingi 467,045,111.

Katika miradi yote hiyo Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Ndugu Amour H. Amour amesisitiza juu ya matumizi bora ya fedha za serikali ambapo aliagiza miradi yote ilingane na thamani ya pesa iliyotumika kuikamilisha.

“Niwapongeze sana kwa kuwa na jengo zuri na kisasa kuliko yote katika Maeneo ambayo Mwenge umeshapita na naomba nisisitize juu ya utoaji huduma bora zenye kufuata weledi  kwa wananchi ili thamani na uzuri wa jengo hili uendane na huduma wanazopata wananchi huku mkizingatia kuwa madaraka mliyonayo yanatokana na uwepo wa wananchi hawa” Aliongeza Amour.

Akiwa katika mradi wa ujenzi wa bweni, bwalo na vyoo ambao umegharimu zaidi ya shilingi milioni 400,  katika shule ya Iguguno Amour alisifu jitihada zilizofanywa na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya kupitia uongozi wa Shule hiyo kwa kazi nzuri ya kuhakikisha wanafunzi wa shule hiyo pekee yenye wanafunzi wa kidato cha tano na sita katika Wilaya ya Mkalama wanakuwa na mazingira mazuri kuanzia sehemu ya kula mpaka kulala ambapo aliwataka wanafunzi hao kusoma kwa bidii.

Mara baada ya kumaliza mbio zake katika Wilaya ya Mkalama, Mwenge wa Uhuru ulikabidhiwa katika Mkoa wa Simiyu makabidhiano yaliyofanyika katika kijiji cha Bukundi wilayani Meatu siku ya Jumanne Julai 4, 2017.

Mwenge wa Uhuru  kwa Mwaka 2017 umebeba ujumbe unaosema “Shiriki Kukuza Uchumi wa Viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu”

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.