• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mwakyembe afika bomani

Imewekwa kwenye: March 12th, 2019

“Umoja wa Nchi za Afrika umeichagua Tanzania kama kitovu cha Ukombozi wa bara la Afrika na kitajengwa kituo maalum cha kumbukumbu za Ukombozi wa bara la Afrika jijini Dar-es-salaam”

Ni kauli iliyotolewa na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Harrison Mwakyembe wakati wa ziara yake aliyoifanya muda mfupi uliopita Wilayani hapa ambapo pamoja na mambo mengine alitembelea Uwanja wa kisasa wa Mpira wa Miguu unaojengwa katika kijiji cha Maziliga na kwenda kwenye boma la Wajerumani lililopo katika kijiji cha Ibaga.

“Hivi karibuni tumepeleka wachezaji wetu wa timu ya Ngorongoro kwenda kujipima kwenye michuano ya Uefa kwa wachezaji wanaendana nao umri na wamerudi wakiwa wamejifunza mambo mengi kwa sababu pamoja na kufungwa na baadhi ya nchi pia kuna nchi nyingine zilizopiga hatua upande wa soka walizifunga ikiwemo Senegal na Australia” Alisema Mhe. Mwakyembe.

Akiwa kwenye Uwanja wa Maziliga, Mhe. Mwakyembe alikipongeza Chama cha Mapinduzi na wananchi wote wanaoendelea kuchangia ujenzi wa Uwanja huo ambapo aliahidi kutuma wataalam kutoka baraza la Michezo la taifa (BMT)  kwa ajili ya kuja kutoa msaada zaidi wa kitaalam ili kuufanya uwe wa kisasa zaidi baada ya kukamilika kwake.

Baaada ya kufika Ibaga Mhe. Mwakyembe pamoja na kusifu na kupongeza  uwepo wa malikale na vivutio vya Utalii Wilayani Mkalama pia alionesha kusikitishwa na uharibifu uliofanywa na wananchi kwenye boma la wajerumani liilopo Ibaga ambao walichimba sehemu kubwa ya eneo la boma hilo kutokana na Imani kuwa Wajerumani walizika tunu mbalimbali chini ya ardhi ya eneo hilo.

“Kwa kweli thamani ya uharibifu mlioufanya hapa ni kubwa kuliko hizo tunu mlizokuwa mnazitafuta kwa sababu mmefuta historia nzuri ambayo hata wajukuu zenu wangekuja kujifunza na kujua asili yao” Alisisitiza Mhe. Mwakyembe.

Mhe. Mwakyembe aliahidi Wizara yake itahakikisha boma hilo linajengwa na kurejeshwa katika asili yake ili kuwawezesha vizazi vilivyopo na vijavyo kujua kwa undani juu ya asili yao.

Awali akimpa taarifa fupi baada ya kumpokea Mhe. Mwakyembe, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Jackson Masaka alisema kuwa Mkalama ni miongoni mwa wilaya zilizojaaliwa kuwa na tunu ya makabila ya asili kabisa barani Afrika yanayoendelea kutunza mla na desturi zake mpaka leo huku akitoa mfano wa kabila la Wahadzabe.

Mara baada ya kutoka katika kijiji cha Ibaga Mhe. Mwakyembe alieleke Wilayani Ikungi kwa ajili ya kuendelea na ziara yake.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.