• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MRADI WA BOOST KUONDOA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU YA KUJIFINZIA NA KUFUNDISHIA KATIKA SHULE ZA MSINGI NCHINI

Imewekwa kwenye: December 14th, 2022


Jumla ya vyumba vya madarasa ya shule za msingi za Serikali elifu 12 (12,000) vinatarajiwa kujengwa  Katika maeneo yenye Upungufu au msongamano wa wanafunzi kupitia mradi mpya wa BOOST unaotekelezwa kwa gharama ya Tsh. Triilioni 1.15  nchi nzima



Kauli hiyo imetolewa  Desemba 13  2022 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)  Angela Kairuki wakati  akifungua Mafunzo ya kuwajengea uwezo wajumbe  wa timu za utekelezaji wa Mradi wa BOOST ngazi ya Mkoa na Halamashauri Uliofanyika Katika ukumbi wa mikutano uliopo Katika shule ya sekondari ya Iliboru Mkoani Arusha.


Kairuki amesema Serikali imeendelea kujenga vyumba vingi vya madasa ya Sekondari ambapo imesaidia kuondoa changamoto ya msongamano  na kwamba kwa sasa Serikali kwa kushirikiana na Benki ya dunia imeanzisha Mradi huo wa BOOST Ili kutatua  Changamoto zinazoikabili elimu ya awali na msingi Nchini kote.


 "kupitia Mradi huu, Serikali itajenga na kukarabati miundombinu ya shule za awali na msingi. Naipongeza serikali kwa Kuanzisha Mradi wa miaka mitano wa kuimarisha ubora wa elimu ya awali na Msingi (BOOST) ambapo katika kipindi hicho, jumla ya shilingi trilioni 1.15 zitatumika" Alisema Kairuki.


Aidha amezitaja changamoto nyingine zitakazotatuliwa na mradi huo ni

baadhi ya shule kutokuwa na mazingira rafiki ya kufundishia na kujifunzia kama vile uwepo wa  miundombinu chakavu,

Upungufu wa vyumba vya madarasa unaosababisha msongamano wa wanafunzi darasani,

baadhi ya wanafunzi wanamaliza Darasa la Kwanza na la Pili bila kumudu stadi za KKK(kusoma, kuandika, na kuhesabu) na  kumaliza darasa la Saba bila umahiri wa somo la Kiingereza.


Aidha ameeleza kwamba Upungufu wa vifaa visaidizi kwa ajili ya kuwezesha ujifunzaji wa wanafunzi wenye mahitaji maalum; na

Upungufu wa vifaa na matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji ni sehemu ya Changamoto zitakazotatuliwa na utekelezaji wa Mradi huo unaotekelezwa kwa kuzingatia matokea.


Hata hivyo Kairuki amesema kwamba OR-TAMISEMI imefanya tathmini ya hali halisi ya miundombinu ya uchakavu kwa Shule zote za Msingi za Serikali zipatazo 17,182 nchi nzima ambapo Matokeo ya tathmini yameonesha kuwa, shule za msingi 1,804 sawa na asilimia 6.3 zina msongamano mkubwa wa wanafunzi.


Waziri ameendelea ameendelea kueleza kwamba  vyumba vya madarasa vipatavyo 7,741 kati ya 147,284 sawa na asilimia 5 vinahitaji kubomolewa na kujengwa upya, wakati   madarasa 35,914 sawa na asilimia 24 yanahitaji ukarabati mkubwa.


Akimalizia hotuba yake Waziri huyo ameeleza kwamba  tathmini hiyo imebaini uwepo wa vijiji au mitaa 1,544 ambayo haina shule za Msingi hivyo kusababisha wanafunzi wa shule za msingi na Awali kukosa Huduma hiyo muhimu.


Wakati huo huo, Kairuki ameagiza  halmashauri zote kuhakikisha wanaandikisha watoto wote wenye umri wa kuanza shule za awali tayari Kwa kujunga na elimu hiyo Januari 2023.


Mkutano umewakutanisha jumla ya Maafisa 226  Kutoka ngazi za Mkoa na Halmashauri ikihusisha Maafisa elimu msingi, Maafisa habari, wagavi ngazi ya Halmashauri wahandisi  na Maafisa Maendeleo ya jamii. Wengine ni maafisa Ustawi wa jamii, waweka Hazina wa Halmashauri, Maafisa elimu Kata, walimu wakuu na waratibu wa mradi wa BOOST.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.