• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA WILAYA YA MKALAMA MHE. MACHARI AKABIDHIWA RASMI OFISINI

Imewekwa kwenye: February 11th, 2023



Mkuu wa Wilaya ya Mkalama  Mhe. Moses Machari  amewaomba Wananchi wa Wilaya ya Mkalama , Watumishi wa Idara na Vitengo Pamoja na  Taasisi zote  Wilayani hapa kumpa ushirikiano wa kutosha ili kuendeleza yale mazuri yaliyofanywa na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya , Mhe. Sophia Kizigo kuhakikisha  Wilaya inasonga  mbele zaidi kimaendeleo.


Ameyassema hayo mapema leo February 4, 2023 wakati wamakabidhiano ya Ofisi  yaliyofanyika katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, ambapo amesema kuwa anamshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuendelea kumuamini  kwa kipindi kingine  na kumteua kuja kuitumikia Wilaya ya Mkalama akitokea Wilaya ya Bukoba na kuahidi kufanya kazi kama timu kwa masilahi mapana ya Wilaya ya Mkalama.

‘’Awali ya Yote ninamshukuru Mwenyezi Mungu kutukutanisha leo, Lakini pia Shukrani zangu zimwendee Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Samia Suluhu Hassani kuona ninafaa kuja kuitumikia Wilaya ya Mkalama , kubwa ninaomba ushirikiano wenu kwasababu kutekeleza majukumu haya ni ‘connection’ , sijaja kutangua torati bali nimekuja kuendeleza yale mazuri yaliyofanywa na Mhe.Kizigo’’ Aliongeza Mhe. Machari.


Aidha alisema kuwa atahakikisha analinda Imani iliyojengwa na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkalama  Mhe. Sophia Kizigo  kwa Wananchi wa Mkalama huku akiwataka watumishi wote kila mmoja kwa nafasi yake kufanya majukumu yake kikamilifu ili kuepuka migongano katika utendaji kazi .


Kwa upande wake aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Sophia Kizigo amewashukuru watumishi wote wa Wilaya ya Mkalama, Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, ,Mwenyekiti wa Halmashauri, Baraza la Madiwani Pamoja na Taasisi zote Wilayani hapa kwa ushirikiano waliompa kwa kipindi chote akiwa Wilayani Mkalama na kuwaomba kumpa ushirikiano huo Mhe . Machari ambaye ndio Mkuu wa Wilaya .


Pamoja na hayo Mhe. Kizigo amemkabishi  Ofisi Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Machari nakumwambia Mkalama iko salama na watu wake ni wachapa kazi  na wanaendelea na shughuli  mbalimbali za maendeleo ikiwa ni Pamoja  na Kilimo, Ufugaji na shughuli za uchimbaji wa madini  hivyo kumuomba kuendeleze alipoishia na kuibua mengine mapya kwa ustawi wa Wilaya ya Mkalama.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.