• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MKOA WA SINGIDA WAJIVUNIA MAPINDUZI MAKUBWA KIUCHUMI NDANI YA MIAKA 61 YA UHURU.

Imewekwa kwenye: December 9th, 2022

Mkoa wa Singida unajivunia mapinduzi  katika sekta ya kilimo  cha mazao ya chakula na biashara ikiwa leo ni maadhimisho ya miaka 61 ya uhuru wa Tanganyika uliopatikana mwaka 1961 chini ya baba wa taifa  Mwalimu Julius Nyerere.


Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Singida Evodius Katare amesema hayo katika hutuba yake wakati  wa maadhimisho ya uhuru ambayo yamefanyika kimkoa katika Wilaya ya Mkalama amesema kuwa Kuanzia mwanzoni mwa miaka ya 1970 mkoa wa Singida haukuwa na uzalishaji toshelevu wa mazao ya chakula na hata ya Biashara  kabla ya maboresho ya teknolojia na dhana za kilimo  jambo liliopelekea kuwa tegemezi na kuwafanya wananchi kuanza kuomba misaada kwa serikali.


"Miaka 61 ya uhuru uzalishaji umeongezeka na kuifanya singida kuwa na chakula cha kutosha ambapo  uzalishaji umeongezeka kutoka tani 197886 mwaka 1990 hadi     tani 649850.02 mwaka 2021 /2022 ongezeko hilo likitokana na jitihada za kuongeza uzalishaji kwa mkoa huu ambao ulikuwa ni miongoni  mwa mikoa ambao ilikuwa inategemea misaada  ya chakula"".Alisema  Katare.


“Mkoa wa Singida ulikuwa ni Miongoni mwa mikoa ambayo ilikuwa na uhaba wa chakula mpaka ikafikia hatua wananchi wakawa wanaomba serikali iwapatie msaada lakini katika miaka 61 ya uhuru kumekuwa na mabadiliko makubwa katika teknolojia na dhana za kilimo jambo ambalo limeongeza uzalishaji wa mazao ya chakula”, Alisema Katare.


Awali Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Asia Messos alitoa salamu za watumishi wa Mkalama alisitiza juu ya uwajibikaji katika kutimiza majukumu ya kila siku kwa watumishi na wananchi kwa ujumla ambapo alisema  kuwa kila mtumishi  ni lazima awajibike katika majukumu yake na  hapaswi kuona ugumu kuwajibika katika utendeji wake.


Aidha aliendelea kutoa mfano kitendo cha aliye kuwa Rais wa awamu ya Pili mzee Ali Hassani Mwinyi cha Kujiuzuru kuwa ni moja ya uwajibikaji na kuwa sio kosa kufanya hivyo pale unapolazimika kufanya .


“Ili tuweze kuwa na maendeleo lazima ndugu zangu watumishi wenzangu tuwajibike kwa kwa kuwajibika tutaweza kutimiza majukumu yetu hivyo uwajibikaji kwetu ni lazima hasa katika kuwahudumia wananchi”,Alisema Mesos.


Aidha aliwataka wananchi wa Mkalama kushiriki na kuunga juhudi za serikali zinazoendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali na sekta tofauti na kuongeza kuwa kupatikana kwa Wilaya ya Mkalama kumerahisisha utekelezaji wa miradi ya  maendeleo katika sekta ya elimu, afya, kilimo , Miundombinu na umeme huku uwepo wa ofisi za kiserikali karibu na wananchi kumerahisha  upatikanaji wa huduma karibu na makazi ya watu.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama James Mkwega alisema kipindi mkalama inategemea kila kitu kutoka wilaya  mama ya Iramba ilikuwa  changamoto katika kupata baadhi ya huduma tofauti na sasa

 Mkalama inajitegemea yenyewe katika kujiendesha kiutawala na hata huduma za kijamii  kama  ambavyo  awali wananchi walikuwa wanazifuata Kiomboi.


“Kuna mafanikio mengi ambayo yamepatika na kutokana na kuwa na wilaya na Halmashauri yapo mambo mengi sana ambayo tulikuwa tunapata mkate mmoja tunagawana na wenzetu wa Iramba  lakini sasa kila mmoja anapata wake, miaka 61 ya uhuru tuna mengi sana ya kujivunia”, Alisema Mkwega.


Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru yamefanyika Leo tar. 9/12/2022 katika viwanja vya Shule ya Sekondari Iguguno huku yakiambatana na kauli mbiu isemayo " AMANI NA UMOJA NI NGUZO YA MAENDELEO YETU ".

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.