• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkoa wa Singida waadhimisha miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania bara kwakujivunia mafanikio kwenye sekta mbalimbali

Imewekwa kwenye: December 8th, 2021

Katika kuazimisha miaka 60 ya uhuru wa Tanzania bara,Serikali ya Mkoa wa Singida na wanachi wake wanajivunia mafanikio makubwa ambayo yametokana na jitihada kubwa zilizofanywa na serikali ya awamu ya kwanza hadi ya sita .

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binirith Mahenge amesema hayo wakati  akihutubia wananchi wa Mkoa wa Singida  katika kilele cha Maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru Kimkoa yaliyofanyika katika , viwanja vya jumbe wilayani Manyoni Mkoani Singida.

Aidha Dkt Mahenge amesema kuwa kwa kipindi cha miaka 60 ya uhuru Mkoa wa Singida umeongeza tija katika sekta mbali mbali zikiwemo za uzalishaji mali na huduma za jamii,utawala bora,ulinzi na usalama,kilimo ,afya,elimu,viwanda na umeme.

‘’kwa kipindi cha miaka 60 ya uhuru tuanjivunia mkoa wetu kuwa na mafanikio mengi na  makubwa ikiwemo kujitosheleza kwa chakula ,ongezeko la uzalishaji wa mazao ya biashara kama ufuta ,Alizeti,Korosho  ,Dengu na vitunguu hii yote ni kutokana na kuongezeka kwa Teknolojia za kisasa kwenye sekta ya kilimo kama vile pembejeo, mbolea ,mbegu bora na hifadhi bora ya mazao’’alisema Dkt Mahenge Rc Singida.

Pamoja na hayo ametaja mafanikio katika uzalishaji wa mazao ya chakula na kusema umeongezeka kutoka tani 197,886 mwaka 1990 na kufikia tani  821,882 kwa mwaka 2020/2021 mara baada ya Mkoa kuainisha uzalishaji wa  mazao  ya chakula ya kipaumbele ambayo ni Mtama,uwele,viazi vitamu na Mihogo ,ambaapo uzalishaji wa mazao hayo yaliongezaka kutoka tani  194,878 kwa mwaka 2005/2006 hadi kufikia tani 395594 kwa mwaka 2020/2021 huku mazao ya biashara yakiongezeka kutoka tani 41,746 mwaka 2005/2006 hadi tani 230,793 mwaka 2020/2021 ambapo zao la alizeti pekee limeongezeka kutoka tani 28,917 kwa mwaka 2005/2006 hadi tani 222,800 kwa mwaka 2020/2021.

Hata hivyo hakusita kutaja mafanikio yaliyopatikana kwenye sekta ya elimu kwa mwaka 1961 hapakuwa na madarasa ya shule za awali ambapo kwa 2021 kuna jumla ya madarasa ya awali 561 na kuongeza  kuwa mkoa umefanikiwa kutoa elimu  kwa  walemavu ambapo kwa mwaka 1961 hapakuwa na shule ya walemavu ukilinganishwa na2021 shule zimeongezeka na kufikia 12.

Sanjari na hayo ametaja mafaniko katika sekta ya afya kuwa  Mkoa una  vituo vya kutolea huduma  za afya   246 ,Hospitali 11 vituo vya afya 20 zahanati 211 huku akiongeza kuwa serikali inaendelea kujenga hospitali za wilaya 3 na kusema Mkoa umepokea fedha  za tozo kiasi cha sh Billion .2.2 kwaajili ya vituo vya afya 9 kupitia mpango wa maendeleokwa ustawi wa taifa  na mapambano ya UVIKO 19 huku Billion 1.9 kwaajili ya ujenzi wa majengo  ya dharura katika hospitali za wilaya ,wagonjwa mahututi na nyumba za walimu.

Dkt Mahenge amewataka wananchi wa Mkoa wa Singida kutumia kikamilifu fursa  za uwekezaji ili kuondokana na umasikini  wa kipato na kuboresha hali ya Maisha ya wananchi  kiuchumi na Kijamii

Kilele cha miaka 60 ya uhuru  wa Tanzania bara Kimkoa  yamefikia tamati leo ta 8/12/2021

Na kitaifa yanatarajiwa kufanyika hapo keshi 9/12/2021 jijini Dar-es-salaamu

Na kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘’MIAKA 60  YA UHURU,TANZANIA IMARA KAZI IENDELEE’’.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.