• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MKALAMA YAPOKEA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA ZAIDI YA MILIONI 300

Imewekwa kwenye: March 14th, 2018

Hamashauri ya Wilaya ya Mkalama leo imepiga hatua kubwa katika sekta ya afya baada ya kupokea vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 345,430,700.00 kutoka taasisi ya HumanBridge yenye makao yake makuu nchini Sweden.

Miongoni mwa Vifaa hivyo ambavyo kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Mkalama vilikabidhiwa kwa Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Jackson Masaka vinajumuisha Meza kwa ajili ya Upasuaji, Vifaa vya upasuaji, Magodoro 25, Vitanda 25, Mashine ya kupima mapigo ya moyo, Vitanda vya kujifungulia kwa wajawazito, Viti vya walemavu wa miguu, vifaa vya kusaidia kutembea kwa wanaosumbuliwa na miguu na vingine vingi.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo, Mgeni rasmi wa hafla hiyo ya mapokezi ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka aliishukuru taasisi hiyo hiyo kwa kuichagua Mkalama kuwa Wilaya ya kwanza kupokea msaada wa aina hiyo ambapo aliwashukuru pia kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuunga mkono jitihada zake za kuboresha sekta ya afya nchini.

“Alipoingia tu madarakani, Mhe. Rais Magufuli alianza na sekta ya afya ambapo aliongeza wodi kwa ajili ya wanawake pale katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili hivyo kitendo hiki ni ishara pekee ya kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais” Alisema Mhe. Masaka.

Mhe. Masaka aliiomba taasisi hiyo kuendeleza ushirikiano waliuoanzisha na Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ambapo aliwaahidi kutunza na kusimamia matumizi ya vifaa tiba hivyo ili kuhakikisha wananchi wa Mkalama wanafaidika ipasavyo na uwepo wa vifaa hivyo katika zahanati na vituo vyao vya Afya pindi wakienda kutibiwa.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mhandisi Godfrey Sanga mbali na kuishukuru taasisi hiyo, alisema kuwa vifaa hivyo vitamaliza mapungufu ya vifaa tiba yaliyokuwepo katika zahanati na vituo vya Afya vilivyopo Wilayani hapa.

“Hata hii thamani ya vifaa iliyotajwa ni kwa mujibu wa vile ambavyo vipo kwenye rejesta ya Bohari ya Dawa ya Taifa (MSD)  lakini kuna vifaa vingine vingi ambavyo tumeletewa hatujajua thamani yake kwa sababu havipo kwenye rejesta ya MSD hivyo thamani ya vifaa tulivyokabidhiwa vinaweza kufika mpaka milioni 400” Alisema Sanga.

Sanga aliongeza kuwa vifaa hivyo vimefika katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama katika wakati sahihi kwa sababu tayari Halmashauri hiyo mbali na kuendelea na ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kinyambuli hivi sasa, halmashauri hiyo katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019 imetenga kiasi cha shilingi milioni 450 kwa ajili ya uboreshaji wa kituo cha Afya cha Mkalama, Shilingi milioni 400 kwa ajili ya uboreshaji wa kituo cha Afya cha Kinyangiri na shilingi milioni 100 kwa ajili ya ukamilishaji wa kituo cha Afya cha Msiu.

Kwa upande wake muwakilishi wa taasisi ya HumanBridge Mchungaji Bahati Kito alisema kuwa jitihada zilizooneshwa na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama katika kuhakikisha vifaa hivyo vinatoka bandarini haraka na kufika kwa walengwa zinapaswa kuigwa na Halmashauri nyingine kwani zimezidi kuwashawishi kutoa misaada mingine zaidi.

“Moja ya Vitu ambavyo viliikatisha tamaa taasisi yetu kutoa misaada mbalimbali nchini Tanzaniani suala la urasimu hasa baada ya mizigo yetu kufika bandarini ambapo baadhi ya makontena tuliyotuma yaliishia kuozea bandarini” Aliongeza Mchungaji Kito.

Mchungaji Kito alimalizia kwa kupongeza juhudi za dhati zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli  katika kulinda rasilimali za Watanzania jambo ambalo linawapa moyo sana washirika wa nchi waliopo nje ya nchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.