• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkalama yaadhimisha siku ya wanawake

Imewekwa kwenye: March 8th, 2019

 

“Badili fikra kufikia usawa wa kijinsia kwa maendeleo endelevu”  Ni kauli mbiu iliyotumika katika maadhimisho ya mwaka huu ya siku ya wanawake duniani ambapo kwa Wilaya ya Mkalama sherehe za maadhimisho hayo zimefanyika katika kata ya Miganga.

Maadhimisho hayo ambayo kwa kiasi kikubwa yalipambwa na burudani mbalimbali zilizobeba ujumbe wa kumsifu mwanamke yalitanguliwa na zoezi la upandaji wa miche ya miti kuzunguka eneo la ujenzi wa kituo cha Afya cha Miganga lililoongozwa na Mgeni rasmi wa sikukuu hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka.

Akihutubia wananchi waliojitokeza katika maadhimisho hayo, Mhe. Masaka alisema kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli imewawezesha kwa kiasi kikubwa wanawake kuonesha uwezo wao katika nyanja mbalimbali za uongozi huku akitoa mfano wa viongozi mbalimbali wanawake walioaminiwa na Rais akiwepo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Naibu spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Tulia Ackson na wengine wengi.

“Kwa mantiki hii Mhe. Rais ameshatuthibitishia kuwa kumbe wanawake pia wanaweza kufanya kazi vizuri kama walivyo wanaume hivyo naagiza hata kwenye shule zetu kuanzia sasa tuondokane na maagizo yanayolenga kuonesha ubaguzi wa kijinsia kwa sababu anachokiweza mwanaume na mwanamke anaweza kufanya” Aliongeza Mhe. Masaka.

Mhe. Masaka pia alitumia fursa hiyo kuwaonya wale wote wanaojihusisha na kuwapa ujauzito wanafunzi ambapo alisema kuwa mtu yoyote atakayebainika kufanya kitendo hicho atashughulikiwa bila kujali itikadi zake za siasa, dini na kabila.

“Kama wewe ni Mwana-CCM na umebainika kumpa ujauzito mwanafunzi tutakushughulikia bila kujali nafasi yako kwenye chama na hali itakuwa hivyo pia hata katika upande wa dini na makabila hatutamuacha mtu” Alisisitiza Mhe. Masaka.

Mhe. Masaka alihitimisha hotuba yake kwa kuwapongeza wanawake kwa kazi nzuri za maendeleo wanazofanya ambapo aliwahimiza kuendelea kujiamini, kujituma na kuwa na uthubutu wa kutumia fursa zilizopo.

Siku ya Wanawake duniani huadhimishwa kila ifikapo Machi 8 ya kila mwaka ambapo huambatana na kauli mbiu mbalimbali zinazolenga kumuinua mwanamke.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.