• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkalama imepiga hatua kubwa-Tulia

Imewekwa kwenye: October 27th, 2018

Naibu spika wa Bunge la  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Daktari Tulia Ackson leo aliongoza viongozi na  mamia ya wananchi wa wilaya ya Mkalama katika harambee ya kuchangia ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu wa Wilaya hiyo.

Harambee hiyo ambayo mpaka kukamilika kwake ilifanikisha kupatikana jumla ya shilingi milioni 61 ilihusisha viongozi mbalimbali wa serikali, viongozi wa vyama vya siasa, wataalam mbalimbali wa Halmashauri ya wilaya ya Mkalama na wananchi kwa ujumla.

Wakati wa harambee hiyo Mhe. Tulia aliwasifu viongozi wote na watendaji wa wilaya ya Mkalama kwa jitihada mbalimbali wanazofanya katika kuhakikisha wilaya hiyo inapiga hatua kadri muda unavyokwenda.

“Najua Mkalama ni moja ya wilaya ambazo hazina muda mrefu sana tangu kuanzishwa kwake lakini nina uhakika kiwango chake cha maendeleo hivi sasa ni kikubwa kuliko baadhi ya Wilaya kongwe zilizoanzishwa muda mrefu hivyo niwapongeze sana kwa hilo” Alisisitiza Mhe. Tulia.

Baadhi ya viongozi waliohudhuria harambee hiyo na kutoa michango yao ni pamoja na Mbunge wa jimbo la Mkalama Mhe. Allan Kiula ambaye alichangia shilingi milioni 4, Mbunge wa viti maalum Mhe. Martha Mlata ambaye alichangia mifuko 150 ya saruji yenye thamani ya shilingi 2,250,000/= na Mbunge wa viti maalum Mhe. Asha-Rose Matembe ambaye alichangia mifuko 50 ya saruji.

Wengine waliochangia katika harambee hiyo ni pamoja na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Mohamedi Mpinga ambaye alichangia mifuko 230 ya saruji, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mkalama ambayo ilitoa kiasi cha shilingi 550,000/=, Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ambaye alichangia bati 98  na shilingi 500,000/=.

Mbali na viongozi hao wengine waliotoa au kuahidi michango yao kwenye harambee hiyo ni pamoja na wakuu wa idara wa Halmashauri ya wilaya ya Mkalama, waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya wilaya hiyo, wafanyabiashara mbalimbali waliopo ndani ya wilaya hiyo na wananchi mbalimbali waliopo ndani na nje ya wilaya hiyo.

Katika hafla hiyo, Mhe. Tulia alipewa rasmi jina la “Nzitu” ambalo asili yake ni kabila la wanyiramba likimaanisha mtoto ambapo mara baada ya kulipokea alimtangaza Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Mkalama Mhe. Lameck Itungi kuwa baba yake rasmi wa kabila hilo.

  

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.