• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkalama yahitimisha zoezi la kupiga chapa

Imewekwa kwenye: September 18th, 2017

Zoezi la kupiga chapa ng’ombe kwa Wilaya ya Mkalama limehitimishwa mapema leo katika kijijicha Gumanga ambapo jumla ya Ng’ombe 192,900 ikiwa ni zaidi ya lengo la awali lililolenga kupiga chapa jumla ya ngombe 127,849.

Akisoma taarifa fupi ya utekelezaji wa zoezi, Afisa Mifugo wa Wilaya ya Mkalama Elias Mbwambo amesema utekelezaji wa zoezi hilo unatokana na sheria namba 12 ya Mwaka 2010 ya usajili, ufuatiliaji na utambuzi wa mifugo ikichagizwa na takwa la soko la kimataifa ambapo ili mifugo iingie katika soko hilo ni lazima ijulikane mahali ilipotoka.

Mbwambo amesema kuwa katika zoezi hili kila mfugaji alitakiwa kulipia shilingi 500 kama gharama ya chapa ambapo fedha hizo zilikuwa zikitumika kwa ajili ya kuratibu zoezi zima mpaka kukamilika kwake.

“Usajili huu umefanyika kwa kutumia code zilizotolewa na Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ambazo ni T MKL na code za vijiji zilizotolewa na Wilaya ambapo vijiji vilipangwa kwa mpangilio wa herufi kuanzia kijiji namba moja hadi 70 na chapa hiyo iliwekwa mguu wa nyuma kulia katikati ya goti na paja” Alisema Mbwambo.

Aidha Mbwambo ameongeza kuwa wafugaji wanaruhusiwa kuwa na alama zao za utambuzi ambapo zitatakiwa kusajiliwa kwanza ndipo wazitumie bila kuathiri zile za serikali na alama hizo zitawekwa mkono wa mbele upande wa Kulia.

Akizungumza muda mfupi kabla ya kufunga rasmi zoezi hilo kwa awamu hii, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kuhakikisha anatenga maeneo ya kulisha mifugo hiyo ili kuondokana na migogoro baina ya wafugaji na wakulima.

“Kumekuwa na mazoea ukifika msimu wa masika  maeneo yote huwa yanalimwa na kusababisha mifugo kukosa maeneo ya chakula jambo ambalo huweza kusababisha mgogoro baina ya mkulima na mfugaji” Alisema Masaka.

Mhe. Masaka ametoa agizo  kwa serikali za vijiji kuwa endapo ng’ombe asiye na chapa atachinjwa, kuuzwa au kusafirishwa nje ya Wilaya hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya mwenye ng’ombe, mchinjaji na mnunuzi wa ng’ombe huyo.

“Wananchi watumie mifugo yao kwa kujiendeleza na kuboresha hali za maisha kwa kufanya shughuli za maendeleo” Alimalizia Mhe. Masaka.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.