• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MKALAMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Imewekwa kwenye: March 8th, 2018

Wilaya ya Mkalama leo imeungana na maeneo mengine yote kusherehekea siku ya kimataifa ya wanawake iliyofanyika katika kijiji cha Mwando yakiwa ni maadhimisho ya tano ya sikukuu hiyo tangu kuanzishwa kwa Wilaya hii.

Katika maadhimisho hayo ambayo mwaka huu yamebebwa na kauli mbiu ya kitaifa isemayo “Kuelekea Uchumi wa Viwanda tuimarishe usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa Wanawake” viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Mkalama na Mkoa wa Singida kwa ujumla walitumia fursa hiyo kuhamasisha wanawake kujitokeza katika fursa mbalimbali na kupiga vita hali ya utegemezi dhidi ya wanaume.

Mbunge wa Viti maalum Mkoa wa Singida Mhe. Asha-Rose Matembe aliwaasa wanawake wote Wilayani Mkalama kujunga kwenye Vikundi ili waweze kukidhi vigezo vya kupatiwa mikopo ya Serikali na taasisi mbalimbali za fedha.

“Niwaombe Sido na taasisi mbalimbali za fedha watembelee vikundi vya wanawake na kutoa elimu ya Ujasiriamali ili fedha wanazokopeshwa ziweze kuwa na tija” Alisisitiza Mhe. Matembe.

Mhe. Matembe pia amepongeza jitihada za wazi zilizooneshwa na wananchi wa Kijiji cha Mwando kwa Kujenga Zahanati ambapo aliunga mkono jitihada hizo kwa kuwaahidi kuchangia mifuko 50 ya Saruji huku 30 akiikabidhi hapo hapo na mingine 20 kuahidi kuitoa ndani ya siku chache zijazo.

Awali kabla ya Kumkaribisha Mgeni Rasmi wa maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mhandisi Godfrey Sanga aliainisha jitihada mbalimbali ambazo serikali imezifanya ndani ya Wilaya ya Mkalama katika kuinua Ustawi wa wanawake ambapo mbali na Asilimia 5 inayokwenda kwenye vikundi vya wanawake vilivyosajiliwa kila Mwezi, Serikali pia inatarajia kukamilisha wodi ya wanawake iliyopo katika Zahanati ya Nduguti ndani ya Siku 60 kuanzia sasa.

“Pia ndani ya Miezi miwili ijayo tunatarajia kukamilisha Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kinyambuli ambacho ndani yake kuna Chumba kikubwa cha Upasuaji kwa wanawake wajawazito jambo ambalo litazidi kuhakikisha usalama wa afya za wanawake waliopo Wilayani Mkalama” Alisisitiza Sanga.

Sanga aliongeza kuwa Bweni la Wanafunzi wa kike katika Shule ya Sekondari Nduguti linatarajiwa kukamilika muda wowote kuanzia hivi sasa hivyo kuanzia Muhula ujao wanafunzi wa Kike wote waliopo shuleni hapo watakuwa wakiishi bwenini jambo litakaloongeza usalama wa watoto wa kike pindi wakiwa shule.

Katika hotuba yake, Mgeni rasmi wa maadhimisho hayo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka ameainisha aina mbalimbali za Unyanyasaji wa wanawake unaoendelea katika jamii likiwemo suala la ndugu wa Marehemu kuchukua Mali pindi mwanamke anapofiwa na mumewe.

“Jambo hili katika Wilaya ya Mkalama sitaki kulisikia na naagiza hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi ya watakaobainika kufanya hivyo” Aliongeza Mhe.Masaka.

Mhe. Masaka aliongeza kuwa kumekuwa na tabia isiyopendeza kwa baadhi ya wanaume ambapo wamekuwa wakiwalaumu wake zao pindi watoto wanapoharibikiwa kimaadili huku wakisahau kuwa jukumu la malezi ya watoto ni la baba na mama kwa pamoja na si mama peke yake.

“Lakini bado kuna baadhi ya kaya ambazo mpaka leo hazimpi mwanamke haki ya kupanga uzazi na bado jamii imekuwa ikifumbia macho badala ya kutoa ushauri unaofaa jambo ambalo linasababisha wanawake kuchoka sana kwa kuzaa mfululizo bila kufuata uzazi wa mpango” Alisema Mhe. Masaka.


Mhe. Masaka alihitimisha hotuba yake kwa kuwataka wanawake wote Wilayani Mkalama kutoona ni jambo la kawaida kwa watoto wao wa kike kupata ujauzito wakiwa shuleni kwa sababu takwimu zinaonesha kiwango cha watoto wa kike wanaopata ujauzito wakiwa Shuleni ni asilimia moja tu hivyo ni lazima wazazi wa watoto hao waungane na hiyo asilimia 99 ili kutokomeza kabisa hali hiyo.

“Mpaka sasa Jumla ya Kesi tatu za ubakaji zimeshafikishwa Mahakamani Wilayani hapa na wahusika wote waliokutwa na hatia wamehukumiwa vifungo” Alimalizia Mhe. Masaka.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.