• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Elimu Mkalama ibadilike kwa vitendo-RC

Imewekwa kwenye: May 18th, 2018

“Elimu ni moyo wa uhakika na hakikisho la uhai wa maendeleo endelevu ya familia, jamii na Taifa kwa ujumla”

Hayo ni maneno yaliyotamkwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Daktari Rehema Nchimbi ambaye alikuwa Mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya Juma la Elimu tukio lililofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.

Mhe. Nchimbi ambaye alimwakilisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo, alitumia fursa hiyo kuwashukuru wadau wote wa elimu chini ya mwamvuli wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMet) ambapo aliwataka watumie maadhimisho ya mwaka ujao kutoa majibu ya tathmini ya utekelezaji wa changamoto zote walizoziona katika Wilaya za Nanyumbu na Mkalama.

“Haiwezekani kila mwaka muwe mnazungumzia changamoto za aina moja hivyo ni lazima muweke mpango mzuri wa kufanya ufuatiliaji wa karibu wa utekelezaji wa changamoto zote mlizoziainisha” Alisisitiza Mhe. Nchimbi.

Mhe. Nchimbi aliushukuru uongozi na wananchi wa Mkalama kwa ujumla kwa kuahidi kubadilisha matokeo waliyoyapata mwaka jana ambapo aliwasisitiza wajikite zaidi kwenye mabadiliko ya vitendo badala ya maneno.

Kabla ya kutangaza kufunga maadhimisho ya juma la Elimu kwa mwaka huu, Mhe. Nchimbi aliendesha harambee ya kuchangia elimu Wilayani hapa ambapo jumla ya shilling 600,000 zilipatikana.

Awali akizungumza maneno machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka alisema kuwa TenMet waliamini Mkalama bado ipo hai ndio maana walifika kuisaidia kuainisha sababu mbalimbali zilizosababisha kutokuwa na matokeo mazuri ambapo aliwaahidi kuwa Wilaya yake haitofanya vibaya tena.

Wakati huo huo Mhe. Masaka alitumia fursa hiyo kuwatakia kila la kheri waislam wote wa Wilaya ya Mkalama katika Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ambapo aliwataka wafanyabiashara wote Wilayani hapa kutopandisha bei za vyakula ambavyo hutumiwa kama futari na daku  katika kipindi hiki.

“Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya itafuatilia kwa karibu sana utekelezaji wa agizo hili na atakayekiuka hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake” Aliongeza Mhe. Masaka.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.