• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MIRADI YA BOOST MINGI IMEKAMILIA KWA 100% MICHACHE IPO KWENYE 90-95% RC SERUKAMBA

Imewekwa kwenye: July 19th, 2023

MIRADI YA BOOST MINGI IMEKAMILIA KWA 100% MICHACHE IPO KWENYE 90% HADI 95%" RC SERUKAMBA '


MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, amefanya ziara ya kukagua miradi ya ujenzi shule mpya za msingi zinazojengwa kwa fedha za BOOST na kuagiza viongozi wa Halmashauri zote za Wilaya Mkoani hapa kuhakikisha ujenzi huo  unakamilika haraka  ili shule hizo zianze kutoa huduma.


Serukamba ameyasema hayo hivi karibuni baada ya kutembelea miradi ya Boost katika Halmashauri za Wilaya za Mkalama,  Iramba , Singida Vijijini na Halmashauri ya Manispaa ya Singida.


Katika Halmashauri ya Wilaya Mkalama  alitembelea na kukagua ujenzi wa shule mpya ya  Ishenga na  kuongea na Wananchi ambapo aliwapongeza viongozi wa Wilaya  kwa kusimamia vizuri miradi hiyo ambayo mingi imekamilika kwa asilimia 100 na michache ipo kati ya asilimia 90 na 95.


"Nichukue nafasi hii kuwapongeza watendaji wenzangu kwa kweli miradi hii imekwenda vizuri, majukumu yetu tuendelee kuyafanya na niwaombe Madiwani na Wenyeviti wa vijiji wahamisishe wananchi kwa ajili ya kufanya usafi katika shule zilizojengwa ikiwa ni pamoja na kupanda miti kuzunguka shule," alisema Serukamba.


Ameongeza kuwa katika kuhakikisha zoezi la upandaji miti linafanikiwa, wanafunzi wapewe miti ya kupanda na kuisimamia jambo ambalo litazifanya shule hizo kupendeza na kuwa na mazingira mazuri.


Serukamba alisema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amejipambanua kwa kufanya kazi kubwa sana ya kuendeleza maisha ya watu kuwekeza kwenye maisha ya watu na vitu vinavyohusu watu.


"Kuwekeza kwenye elimu ni kuwekeza kwenye mtu mmoja mmoja, ukiwekeza kwenye afya umewekeza kwenye afya ya mtu mmoja kimsingi Mhe. Rais amefanya kazi kubwa sana sana, pia hajaacha sekta za uchumi kama umeme, barabara kuna kazi kubwa sana imefanyika," alisema Serukamba.


Ameongeza kuwa katika sekta ya umeme Mkoa wa Singida una vijiji 441 itakapofika Juni 2024 kila Kijiji kitakuwa kimepata huduma ya umeme na kumpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri alizofanya kwa Mkoa wa Singida.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.