• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Makamu wa Rais kuinufaisha Mkalama

Imewekwa kwenye: September 5th, 2018

Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Mfuko wa Dunia wa Mazingira (GEF) na Mfuko wa kimataifa wa maendeleo ya kilimo (IFAD) inatarajia kuipa fursa ya kipekee wilaya ya Mkalama baada ya kukamilika kwa utekelezaji wa mradi wa Kurejesha Ardhi iliyoharibika na kuongeza uhakika na Usalama wa Chakula katika maeneo kame ya Tanzania (LDFS).

Mradi huo unaoendelea katika nchi 12 barani Afrika zilizopo kusini mwa jangwa la Sahara unatarajiwa kutekelezwa katika vijiji vya Mpambala, Nyahaa, Lugongo na Mkiko vilivyopo katika kata ya Mpambala.

Kupitia mradi huo wananchi wa Mpambala watapata fursa ya kushiriki moja kwa moja kupitia kamati za uwakilishi za vijiji zitakazoshirikisha jinsia zote ambapo zitakuwa na kazi ya kupanga na kusimamia maliasili zilizopo kati ya vijiji kwa kukubaliana katika upangaji na matumizi yanayozingatia usawa na kuandaa miongozo.

Mradi huo unaotarajiwa kuanza mapema mwezi ujao  pia utaipa serikali fursa ya kutambua teknolojia na maeneo yanayofaa kwa uvunaji wa mvua na  maeneo ya vyanzo vya maji ambapo teknolojia hiyo itasaidia kupunguza upotevu wa maji na kuongeza uzalishaji hasa kipindi cha kiangazi kwa wananchi wa kata ya mpambala.

Wananchi wa vijiji vya kata ya Mpambala pia watapatiwa mafunzo ya shamba darasa kuhusu kilimo hifadhi na mbinu bora za kilimo rafiki kwa mazingira, uboreshaji na urutubishaji wa udongo, mbinu za kilimo misitu, kilimo cha makinga maji, kilimo cha mzunguko na usimamizi shirikishi wa kudhibiti wadudu na magonjwa ya mazao.

Mafunzo hayo yataenda sambamba na kuwasaidia wakulima hao upatikanaji wa mbinu bora za kilimo na pembejeo  katika mashamba darasa yatakayoanzishwa.

Mbali na Mkalama wilaya nyingine zinazotekelezwa mradi huu hapa nchini ni Kondoa (Dodoma), Nzega (Tabora), Magu (Mwanza) na Micheweni (Kaskazini Pemba).

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.