• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MADUME BORA YA MBEGU KULETA MAGEUZI YA KIUCHUMI WILAYANI MKALAMA

Imewekwa kwenye: April 6th, 2023

Waziri wa Mifugo na Uvuvi   Mhe. Abdallah Ulega amesema kuwa  uwepo wa madume bora ya kisasa ya Ng’ombe  aina ya BORAN yatafungua fursa za kiuchumi  kwa  wafugaji  Wilayani Mkalama  kwani  itaongeza uzalishaji   wa nyama  utakaopelekea  wafugaji  kupata soko ndani  na nje ya Nchi .


Ameyasema hayo  mapema  leo  April 6, 2023 katika hafla fupi ya kukabidhi  mbegu bora ya madume  Arobaini  (40) ya Ng’ombe iliyofanyika katika kijiji  cha Iguguno Kata ya Iguguno Wilayani Mkalama.

Aidha Mhe . Ulega ameongeza  kuwa  Serikali imedhamiria kuboresha Sekta  ya Mifugo  na kuwainua wafugaji  ili kuhakikisha wanaongeza kipato chao kupitia mifugo itakayoleta mageuzi kiuchumi kwa mtu  mmoja mmoja , Wilaya , Mkoa  pamoja na Taifa.


‘’Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais  Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kipindi cha miaka miwili   imedhamiria kuinua Sekta ya Mifugo  Nchini na kutoa zaidi ya Shillingi  Million 800 kununua madume  bora ya mbegu  ya Ng’ombe  366 ambayo leo hii inamgusa hadi mwananchi wa Mkalama lengo likiwa ni kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja na kuleta mageuzi ya kiuchumi Wilayani hapa’’ Aliongeza Mhe. Ulega


Aidha alitumia hafla hiyo  kuwataka wafugaji kutumia madume hayo vizuri kutokana na malengo yaliyokusudiwa na serikali ili kuunga mkono  juhudi hizo zinazokusudia  Ng’ombe hao kupandisha Ng’ombe jike ili kuweza  kupata mbegu bora itakayoleta faida kwa wafugaji huku akiwaonya kutofanya  Ng’ombe hao kuwa kitoeo.


Awali akimkaribisha Waziri,  Mkuu wa Wilaya ya Mkalama,  Mhe. Mosses Machali  ameishukuru serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi  kutoa  madume ya Mbegu 40 katika Wilaya ya Mkalama ambayo yatagaiwa kwa Vikundi Arobaini  vya Wafugaji ambapo ameahidi kuwa watahakikisha wanasimamia vizuri Madume hayo ili kufikia malengo tarajiwa ya kuwa na mifugo bora  yenye mazao mengi yatakayochangia kuongeza na kukuza  Uchumi  kwa  kaya za wafugaji  na uchumi wa taifa na kuongeza uzalishaji wa mazo ya mifugo.


Naye Mbunge wa jimbo la Iramba Mashariki Mhe. Francis Isack Mtinga  aliongeza kuwa Halmashauri  ya Wilaya ya Mkalama ni miongoni mwa Halmashauri 8 kati ya Halmashauri 186 Nchini zilizopokea Madume hayo na kusema ni bahati ya pekee , huku akiomba Serikali kuongeza majosho kwaajili ya kuogesha mifugo ili  Wilaya ya Mkalama isiwe na  magonjwa yanayoshambulia mifugo sambamba na kuomba ujenzi wa soko kubwa la Mifugo likalopelekea wafugaji kuuza mifugo yao hapa Wilayani na kuongeza vipato vyao pamoja na kuongeza pato la Halmashauri kutokana na kupata ushuru kupitia soko hilo.


Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wananchi Wilayani hapa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mhe. James Mkwega ameishukuru serkali  kuwajali  wananchi  wa Wilaya ya Mkalama kupata Mbegu bora za Madume ilikuongeza uzalishaji na upatikanaji wa nyama wilayani hapo ambapo ameomba kujengwa kwa machinjio Wilayani ili Nyama hizo ziweze kuchinjwa mahali pazuri na kwa usalama ili  kulinda afya za walaji.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.