• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MADIWANI TUIJENGE NDUGUTI 'MHE MKWEGA

Imewekwa kwenye: August 1st, 2023

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mhe. James Mkwega amewataka Madiwani kushirikiana pamoja kuijenga  Kata ya Nduguti kwani ndio Makao Makuu ya Wilaya.


Ameyasema hayo mapema leo (Agosti 1,2023) katika Baraza la Madiwani la Robo ya Nne kwakipindi cha April- Juni 2023 ambalo lilihusisha  kamati mbalimbali kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa majukumu ya Serikali kwa kipindi cha miezi Mitatu.

Mhe. Mkwega alitumia nafasi hiyo kuwataka  madiwani kwa umoja wao kuungana pamoja kuisemea Kata ya Nduguti iweze kupata miradi mingi ya maendeleo kwani ndio Taswira na kioo cha Wilaya.


‘’kwa kuwa Nduguti bado ni Kijiji tunahitaji kwanza Taasisi zijae hapa mjini ili watu wakija waone kuna Shule ya Kidato cha Tano na Sita, Shule Maalum na Soko la Kimkakati lipo mjini hapa, Kuwa na Makao Makuu ya Wilaya ni neema, tusiipime Nduguti na Kata nyingine kwa kila jambo huu mji tutaudhoofisha’’ Alisistiza Mhe.Mkwega


Pamoja na hayo aliwataka Maafisa Tarafa kuisaidia Halmashauri kuzunguka Shuleni kuhamasisha suala la Lishe  pia kuhakikisha Kata zinakuwa na ratiba ya kufanya mikutano kwa wakati ili jamii ipata taarifa zote zinazofanywa na Serikali inayoongozwa na Rais Shupavu wa awamu ya Sita Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Hussein Mwatawala , Kaimu Afisa Tawala Mkoa wa Singida,  alitumia nafasi hiyo kuupongeza Uongozi wa Wilaya ya Mkalama kushika nafasi ya pili  katika ukamilishaji wa Miradi ya BOOST pamoja na kushika nafasi ya kwanza katika ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa asilimia 109 hivyo kuwataka kuendelea na Ushirikiano waliona katika kuchochea Maendeleo ya Wilaya.


Akimwakilisha Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Afisa Tarafa ya Kinyangiri, Bw. Isack Kimaro amesisitiza  wananfunzi wote wa  shule za Msingi na Sekondari kupata chakula shuleni, hivyo waheshimiwa madiwani  wanawajibu wa kuhamasisha  jamii kuchangia chakula.


Mwenyekiti wa CCM wilaya, Bw. Lameck Itungi Amepongeza Uongozi wa wilaya kwa kutekeleza miradi ya maendelea kwa weledi na kuwataka Viongozi kukemea upotoshaji unaoendelea kwa baadhi ya watu kuhusu uwekezaji wa Bandari.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.