• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Maafisa habari wapatiwe Vifaa ndani ya miezi mitatu-Simbachawene

Imewekwa kwenye: March 28th, 2017

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Twala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)  Mhe: George Simbachawene amewaagiza Wakuu wa Mikoa na Wakurugenzi wa Halmashauri wa Wilaya wote kuhakikisha wamewanunulia maafisa habari waliopo katika ofisi zao zana zote zitakazowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kitaalamu zaidi ndani ya kipindi cha miezi mitatu kuanzia jana.

Mhe: Simbachawene ameyasema hayo jana wakati wa Hafla ya Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa yote na Halmashauri 185 za Tanzania bara ambazo zimetengenezwa kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID) chini ya usimamizi wa TAMISEMI na Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo.

“Bila kuwapa vitendea kazi maafisa hawa, juhudi zote za serikali katika kukamilisha zoezi hili zitakuwa hazina tija yoyote kwa sababu mtu anayetakiwa kuhakikisha anatimiza lengo tunalolitaka atakuwa hajawezeshwa kikamilifu na ikumbukwe hivi sasa mitandao ya kijamii imemfanya kila mtu kuwa ni mtoa habari hivyo ni lazima tumtofautishe mtaalamu wa serikali na mwandishi wa kwenye mitandao ya jamii” Amesema Simbachawene.

Mhe: Simbachawene Ametoa rai kwa maafisa habari na maafisa Tehama kote nchini kuhakikisha tovuti hizo zinakuwa na taarifa zinazoenda na wakati muda wote na zitoe majibu kwa wananchi walio mbali na ofisi za Serikali katika halmashauri zao.

Naye Waziri wa Habari, Sanaa,Utamaduni na Michezo Mhe: Harrison Mwakyembe amesema kuwa Nchi ya Tanzania jana imeweka historia kubwa sana tangu ilipopata Uhuru kwa sababu haijawahi kupiga hatua hiyo kubwa kabisa.

“Hata Wizara yangu ambayo ipo kwa muda mrefu sana, haikuwa na tovuti yake lakini sasa hivi kupitia zoezi hili imefanikiwa kupata tovuti yake, hongereni sana wote mliofanikisha hili” Amesema Mwakyembe.

Mhe: Mwakyembe aliwataka maafisa habari wote Nchini kuhakikisha tovuti hizo zinakuwa na taarifa sahihi na zinazoenda na wakati ili kukidhi haja ya mwananchi ambaye ndio mlengwa mkuu wa taarifa zinazowekwa humo.

“Tovuti hizi hazitakiwi kugeuka magofu ya kuhifadhia taarifa zilizopitwa na wakati bali zinatakiwa kuwa jokofu la kuhakikisha habari zinakuwa mpya wakati wote na hapa ndio tutatumia kama kipimo kikubwa kwa maafisa habari wote Nchini” Alimalizia Mwakyembe.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.