• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Maadhimisho ya Wiki ya Sheria Mkalama na Iramba

Imewekwa kwenye: February 6th, 2019

“Kuanzia sasa Ofisi za upelelezi za Iramba na Mkalama tumekubaliana mashauri ya ubakaji, utiaji mimba wanafunzi na uharibifu wa mali za umma  yapelekwe mahakamani moja kwa moja bila kusubiri kukamilika kwa uchunguzi wa polisi ili wahanga wa matukio hayo wakatoe ushahidi mahakamani moja kwa moja na haki iweze kutendeka mapema.”

Kauli hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya  Wilaya Iramba na Mkalama  Mhe. Christopher Charles alipokuwa akizungumza wakati wa maadhimisho ya  kilele cha Wiki ya Sheria nchini kwa Wilaya za Mkalama na Iramba yaliyofanyika leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa  Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.

Mhe. Charles alibainisha kuwa moja ya changamoto kubwa zinazoukabili mhimili wa mahakama kwa mkoa wa Singida ni kukosekana kwa Ofisi ya Mkemia Mkuu ndani ya Mkoa huo jambo linalosababisha kuchelewa kukamilika kwa kesi zinazohitaji uthibitisho kutoka kwenye ofisi yake.

“Mtu anaweza kukamatwa na bangi au unga aina ya “cocaine”, Mahakama haiwezi kutoa hukumu ya kesi hiyo bila kuwa na uthiibitisho kutoka kwa mkemia Mkuu kuwa vithibiti alivyokamatwa navyo ni vya dawa za kulevya au la kwa hiyo mpaka visafirishwe na majibu kurejea inachukua muda mrefu sana” Aliongeza Mhe. Charles.

Mhe.  Charles alisema kuwa ili kauli mbiu ya Wiki ya sheria kwa mwaka huu iweze kutimia kwa vitendo ni lazima  Mkalama iwe na jengo lake la Mahakama ya Wilaya hivyo aliuomba uongozi wa Wilaya hiyo kuharakisha taratibu za utekelezaji wa azma hiyo inayolenga kuwarahisishia wananchi kupata huduma kwa wakati.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iramba ambaye pia ni Mwenyekiti wa wakuu wa wilaya zote za Mkoa wa Singida Mhe. Emanuel Luhahula alivipongeza vyombo vya Ulinzi na Usalama Wilayani Iramba kwa kutimiza wajibu wao ipasavyo ambapo aliwataka kuendelea na kasi hiyo ili wananchi wake wapate haki zao kwa wakati.

“Kuna kipindi vitendo vya Rushwa vilikithiri sana Iramba lakini nilipotangaza Vita dhidi ya wanaopokea au kutoa rushwa, vitendo hivyo vimepungua kwa kiasi kikubwa sana” Alisisitiza Mhe. Luhahula.

Naye mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka aliitaka mahakama kuendelea kuhakikisha haki inatendeka katika mashauri mbalimbali yanayosikilizwa ili kuzidi kuongeza Imani ya wananchi dhidi ya mhimili huo muhimu.

Madhimisho ya Wiki ya sheria mwaka 2019 yalibebwa na kauli isemayo “Utoaji haki kwa wakati: Wajibu wa mahakama na wadau”.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.