• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Kongamano la Usafi lafana

Imewekwa kwenye: February 9th, 2019

Katika kuhakikisha wanafunzi wa Wilaya za Mbulu na Mkalama wanaondokana na maradhi yatokanayo na uchafu wa mazingira na ukosefu wa vyoo bora, Shirika lisilokuwa la serikali linalojulikana kama ‘‘Norwegian Church Aid’’ kupitia mradi wake wa 4CCP leo liliratibu kongamano la Usafi lililoshirikisha watendaji mbalimbali wa Halmashauri za Wilaya hizo wakiongozwa na Wakurugenzi watendaji, maafisa elimu msingi na sekondari, maafisa elimu kata, maafisa afya, wakuu wa shule na walimu.

Shirika hilo ambalo tangu mwaka 2016 limekuwa likiendesha kampeni ya kuhakikisha kwenye shule za Wilaya ya Mbulu na Mkalama kunakuwa na matumizi ya maji safi na salama, Usafi wa vyoo, na unawaji mikono kwa usahihi baada ya kutoka chooni inayojulikana kifupi kama “SWASH” liliandaa kongamano hilo kwa lengo la kuwakutanisha wadau wote wanaowajibika na afya za wanafunzi wakiwa shuleni ili kuweza kuwafikishia moja kwa moja changamoto wanazopata katika kuendesha kampeni hiyo.

Akizungumza na viongozi hao mratibu wa kampeni ya “SWASH” kutoka shirika la NCA Bw. Zakayo Makobelo alisema kuwa shirika hilo kwa mwaka huu litajikita kwenye mafunzo ya mtumizi mengine ya maji (Multiple Use of Water), kampeni ya usafi wa mazingira na kuimarisha klabu za Usafi wa Afya pale ambapo zipo na kwenye maeneo ambayo hazipo shirika litahakikisha klabu hizo zinaanzishwa.

Kwa upande wake Mgeni rasmi wa kongamano hilo kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Bw. Omary Mtamike aliushukuru uongozi wa shirika hilo kwa kampeni yao ya kuhakikisha afya za wanafunzi wakiwa shuleni zinalindwa ipasavyo ambapo aliwaomba kuongeza klabu nyingi zaidi ili kuondokana kabisa na maradhi yatokanayo na uchafu kwenye shule za Wilaya za Mkalama na Mbulu.

“Wakati mnaanza kampeni hii mwaka 2016,  Wilaya ya Mkalama ilikuwa na klabu moja tu ya Swash ambayo ni shule ya Msingi Nkinto lakini mpaka kufikia mwisho wa mwaka jana mlikuwa mmefanikiwa kuongeza klabu nyingine 13 na kuifanya Wilaya ya Mkalama kuwa na klabu 14, Hongereni sana kwa hilo” Aliongeza Bw. Mtamike.

Shirika la NCA limekuwa limekuwa likitekeleza miradi mbalimbali ya kuboresha huduma za jamii katika Wilaya za Mbulu na Mkalama ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ya maji, elimu na mazingira.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.