• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Kitunguu cha Mkalama ni cha Kimataifa- Nchimbi

Imewekwa kwenye: August 7th, 2017

Mapema leo jioni  Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Daktari Rehema Nchimbi ametembelea banda la halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ambapo ametoa maagizo mbalimbali kwa Mkurugenzi, Mwenyekiti wa Halmashauri na Afisa Kilimo wa Wilaya kuhakikisha maonesho yanayokuja ya Nanenane yanakuwa na tija kubwa hata kwa mwananchi wa Mkalama ambaye hajabahatika kufika katika Maonesho ya kikanda.

Mhe. Nchimbi amesema kuwa Kuanzia sasa Wilaya ya Mkalama itenge eneo kubwa ambalo litawekwa vipando ambavyo vitakuwa hapo kwa kipindi cha Mwaka mzima ili wananchi ambao hawatopata fursa ya kushiriki katika maonesho ya kikanda na kitaifa watumie nafasi hiyo kwenda kujifunza kilimo bora na cha kisasa.

“Ninaposema mwaka mzima namaanisha katika maeneo hayo mfanye utaratibu wa kuchimba visima kwa sababu mvua haipatikani mwaka mzima na hapo wananchi kutoka sehemu mbalimbali watafika na kupata elimu tena vipando hivyo mnaweza kuviita ‘NaneNane Mkalama Mubashara’ mkimaanisha wananchi watakuja kujifunza  moja kwa moja kutoka shambani” Amesisitiza  Mhe. Nchimbi.

Mhe. Nchimbi amesema kuwa kitendo hicho kitawafanya wananchi wote wa Mkalama waone umuhimu wa sikukuu ya NaneNane kwa sababu pamoja na kutofika katika maonesho ya kikanda na kitaifa bado watakuwa wamepata elimu inayofanana na wale waliohudhuria maonesho hayo kikanda na kitaifa.

“Ikifika Mwezi Septemba nitafuatilia hili ili nijue kama utekelezaji wake umeanza” Ameongeza Mhe. Nchimbi.

Mhe. Nchimbi pia ameagiza  halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ihakikishe imetangaza bidhaa zake kila inapotimia robo mwaka na bidhaa hizo zisiishie kutangazwa katika redio za mikoani tu bali ununuliwe muda katika vituo vya Televisheni pia.

“Kupitia vipindi hivyo tangazeni kila kinachozalishwa Mkalama vikiwemo vitunguu, asali, nyanya na kwa kufanya hivyo mtakuwa mmetangaza soko la Mkalama sio tu kitaifa bali kimataifa” Amesisitiza Mhe. Nchimbi.

Mhe. Nchimbi amesifia Vitunguu vinavyozalishwa katika Wilaya ya Mkalama ambapo amesema vina ubora wa kimataifa na hata sokoni ndio vitunguu vinavyopewa kipaumbele kuliko vitunguu vinavyozalishwa katika maeneo mengine.

“Kuna baba mmoja ni mstaafu wa jeshi alilima vitunguu katika Mkoa wa Morogoro tena vitunguu vizuri tu lakini alipovipeleka sokoni alikataliwa na kuambiwa vitunguu pekee vinavyonunuliwa hapo ni vile vinavyotoka Mkoani Singida kwa hiyo tangazeni sana bidhaa zenu kwa sababu zina thamani kubwa sana sokoni” Alimalizia Mhe. Nchimbi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.