• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Kilimo cha zao la Pamba kiwanufaishe wakulima Wilayani Mkalama

Imewekwa kwenye: October 21st, 2021

Wakulima wameshauri kulima zao la Pamba kwa kuzingatia Kilimo cha kisasa na kufuata kanuni Bora za kilimo  ili kuongeza thamani  katika zao hilo na kujikwamua na hali duni ya maisha.


Hayo yamesemwa na Bw. Juma Salum Mkaguzi wa zao la Pamba kwa Wilaya ya Mkalama na Iramba wakati akitoa mafunzo elekezi ya namna ya kulima zao la Pamba kwa tija katika Vijiji vya Lugongo,Nyahaa na Mpambala  Kata ya Ibaga wilayani Mkalama Mkoani Singida.


Bw.Salum amesema kuwa zao la Pamba litamkwamua Mkulima katika hali duni ya maisha endapo watazingitia kanuni za kilimo ikiwa ni pamoja na kuandaa shamba mapema,kuweka mbolea pamoja na kupanda kwa wakati.


"Tumekuja kuhamasisha wananchi kulima zao la Pamba lengo likiwa ni kuongeza Tija kwenye zao hili  kwa kuzingatia kipindi sahihi  cha upandaji wa zao la Pamba ambapo tunashauri kuanzia tar 15 /11 hadi tar 15/12 Mkulima awe amepanda mbegu kwa kuzingatia vipimo sahihi pia kupalilia kwa wakati  pamoja na kuvuna kwa wakati ili kuongeza tija katika uzalishaji wa pamba " aliongeza Bw.Juma Salum Mkaguzi wa zao la Pamba.


Aidha ameongeza kuwa ili kuongeza uzalishaji wa zao la Pamba wilayani Mkalama serikali kwakushirikiana na Bodi ya Pamba  Tanzania  itatoa mbegu kwa wakulima kwa Mkopo pamoja na kutoa elimu kwa maafisa Ugani na wakulima  ili wawe mabalozi kwa wengine.


Baadhi ya wakulima wa Vijiji vya Lugongo Nyahaa na Mpambala wameishukuru serikali kupitia bodi ya pamba kutoa elimu ya uhamasishaji wa kilimo cha zao la pamba ambapo wamesema kuwa watazingitia kanuni walizofundishwa huku wakiiomba serikali kuhakikisha wanapeleka pembejeo mapema pamoja na kuwa na soko la uhakika.


Frank Lupogo kutoka shirika la Biosustain wanaojihusisha na ununuaji wa pamba  amewahakikishia wakulima kuwa watanunua Pamba kutokana na bei elekezi itakayopangwa hivyo kuwataka kuondoa hofu kwani uhakika wa soko upo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.