• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

KILA MMOJA AKAWAJIBIKE' DC MACHALI'

Imewekwa kwenye: December 21st, 2023


Maafisa elimu, Waratibu elimu Kata pamoja na walimu wote wametakiwa kutathimini utendaji kazi wao na kuekeleza nguvu zao katika majukumu yao ili kuhakikisha wanainua kiwango cha taaluma wilayani Mkalama na kuongeza ufaulu.


Kauli hiyo imetolewa mapema leo Disemba 21, 2023 na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Moses Machali katika kikao cha tathimini ya ufaulu wa wa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi iliyofanyika katika ukumbi wa Sheketela uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.


Mhe. Machali amesema kuwa endapo kila mmoja kwa nafasi yake atasimamia majukumu kikamilifu watachoche ongezeko la ufaulu kwa wanafunzi pamoja na kujiweka kwenye nafasi nzuri Kimkoa.


‘Nendeni mkasimamie majukumu yenu kikamilifu Afisa elimu ukitimiza majukumu, Mratibu elimu kata na walimu kwa pamoja mkiwajibika kwa nafasi zenu mtachochea ufaulu Wilayani hapa’’ Mhe. Moses Machali



Pamoja na hayo Mhe. Machali amewataka waratibu elimu na walimu wa shule zote kutumia Ardhi ya shule katika kipindi hiki cha Masika kulima mazao kwaajili ya chakula cha wanafunzi yatakayopelekea kupata chakula shuleni kwa wanafunzi wote ili kupata utulivu wa akili wanapokuwa masomoni.



Aidha, Mhe. Machali amewapa mwezi mmoja waratibu elimu wote wanaoishi Nje ya maeneo yao ya kazi kuishi mahala wanakufanyia kazi ili kuongeza ufanisi wa usimamizi wa majukumu yao.



Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Bi. Asia Messos amesema kama Wilaya imejiwekea mikakati ya kuimarisha na kuboresha usimamizi wa mifumo ya ufuatiliaji ikiwa ni pamoja na kutoa motisha kwa wanafunzi  na walimu wanaofanya vizuri katika taaluma,  pamoja na kuwatambua wanaofanya vibaya kwa  kuwapa zawadi hasi itakayowafanya wajitathimini na kuongeza juhudi.


 Bi. Messos  amewaagiza watendaji wa kata kushirikiana na waratibu elimu  pamoja na kamati za shule  kuwachukulia hatua za kisheria  wazazi wanaoshindwa kusimamia mahudhurio ya  watoto wao ili kuondoa tatizo la utoro kwa wanafunzi ambapo imeonekana ndio tatizo kubwa linalochangia  kushuka kwa kiwango cha ufaulu Wilayani hapa.



Awali akisoma taarifa Kaimu Afisa Elimu Shule ya Msingi Mwl. Amina Irumba, amesema kuwa  Halmashauri imeongeza ufaulu kwa asilimia 2.7 kwa kupata 68.30% mwaka 2023  ukilinganisha na mwaka 2022 ambapo ufaulu ulikuwa 65.52% ambapo ameongeza kuwa  ufaulu kimasomo  unaonyesha watahiniwa  wamefaulu kwa kiwango cha juu  kwa somo la Kiswahili 77% huku somo  la Kiingereza  na Hisabati ikiwa chini  ya 50%.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.