• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

KAPU LA MAMA LAKAMILISHA MADARASA 18 WILAYANI MKALAMA.

Imewekwa kwenye: December 22nd, 2022


Mkuu wa wilaya ya Mkalama Mhe. Sophia Kizigo amewataka wazazi kuwekeza kwenye elimu ili kuwa na Taifa la wasomi watakaoshika nyadhifa  mbalimbali  Nchini.


Mhe. Kizigo ameyasema hayo mapema leo Disemba 22 2022  katika hafla ya kupokea madarasa 18  wilayani hapo   katika Shule ya Sekondari Iguguno iliyopo Kata ya Iguguno.


Aidha Mhe. Kizigo amewataka wazazi wote Wilayani kwake kuunga juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita ambayo imekuwa ikitoa fedha nyingi katika Miradi ya Elimu kwa kuhakikisha  ifikapo mwezi Januari mwakani kila mtoto aliyechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza anaripoti shuleni mapema.


‘’Serikali ya awamu ya sita inatujali sana Wananchi wa Wilaya ya Mkalama leo nimepokea madarasa 18 na Ofisi moja ya walimu hakika Mama ameupiga mwingi ninaomba tuhakikishe tunawekeza kwenye elimu,  unajisikiaje Mkuu wa wilaya akatoka mkalama? Mtajisikiaje Watoto wenu wa Mkalama wakawa Mahakimu na wataalamu wa kilimo watakaolima kwa tija kwa masilahi ya Wilaya?..Amesema Mhe. Kizigo


Mhe. Kizigo amewataka wazazi wilayani kwake kutowatumikisha watoto kwenye shughuli mbalimbali za kiuchumi ambapo amebainisha kuwa kufanya hivyo ni kurudisha nyuma juhudi za Serikali ambazo zinalenga kutoa elimu bora kwa watoto.


‘’Ninaomba mtafute watu wengine wa kuchunga  sio Watoto wenu waacheni waende shule la sivyo madarasa haya mengi niliyopokea leo yatakosa maana kama Watoto wenu hawataenda Shule’’ Aliongeza  Mhe. Kizigo.


Awali akitoa taarifa ya utekelezaji  wa ujenzi wa madarasa hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Bi. Asia Messos amesema Halmasahauri yake ilipokea fedha kiasi cha Shilingi Milioni  340  kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 17 vya madarasa ya wanafunzi wa kidato cha kwanza waliochaguliwa kujiunga na Shule kwa mwaka 2023 na tayari madarasa hayo yamekamilika na yapo tayari kutumika.


Aidha Bi Mesos ameongeza kuwa kutokana na ushiriki wa Wananchi kujitoa nguvu kazi  fedha  zilizotolewa  zimechonga viti na meza seti 375, kuongeza chumba kimoja cha darasa  katika Shule ya Sekondari Iguguno  pamoja na ofisi moja ya walimu  hivyo kufanya jumla ya madarasa 18 na Ofisi ya walimu.


Nao baadhi ya wananchi walioshiriki tukio hilo wameishukuru serikali ya awamu ya Sita kwa kujenga madarasa hayo ambayo wamedai yatainua kiwango cha taaluma Wilayani Mkalama huku wakiiomba serikali kuongeza walimu ili kuweka uwiano sawa kati ya wanafunzi na walimu.


Shule zilizopata Mradi huo ni  Shule ya Sekondari Chemchem iliyopo kata ya Mpambala, Malaja iliyopo kata ya Nkalakala, Shule ya Sekondari Seth Benjamini iliyopo kata ya Nkalakala, Selenge Kata ya Mwanga, Gracemesaki kata ya Kinampundu, Kikhonda Kata ya Kikhonda, Kinto Kata ya Nkinto, Iguguno kata ya Iguguno, Kinyangiri Kata ya Kinyangiri pamoja na Shule ya Sekondari ya Ibaga Kata ya Ibaga.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.