• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA IMEKUJA KWA MUDA MUAFAKA

Imewekwa kwenye: January 12th, 2024


KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA IMEKUJA KWA MUDA MUAFAKA' WANANCHI MPAMBALA WANENA'

Wananchi wa Kata ya Mpambala katika Vijiji vya Mpambala, Mkiko na Lugongo wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Kampeni yake ya msaada wa kisheria (Mama Samia Legal Aid Compaign) kwani imelenga kutatua matatizo yao mbalimbali ambayo walikuwa hawajui pakuyapeleka.

Wamesema hayo mapema leo Januari 12, 2024 kwa majira tofauti tofauti baada ya timu ya wataalamu kufika katika maeneo hayo na kueleza namna Kampeni hiyo itakavyoenda kufanya kazi hususani kutatua migogoro kwenye ngazi ya jamii ikiwepo inayohusu masuala ya Ardhi, Ndoa , Mirathi pamoja na matunzo kwa watoto.

Pamoja na hayo wamesema kuwa kampeni hiyo imefika kwao kwa muda muafaka kwani walikuwa wanashindwa ni wapi wapeleke matatizo yao na kuongeza kuwa  watatumia vyombo vya utatuzi vilivyopo kwenye vijiji pamoja na kata zao ikiwa ni pamoja na kutumia vizuri mabaraza ya kata katika kutatua migogoro ya Ardhi ambayo imeonekana kwa asilimia kubwa imekithiri katika maeneo yao pamoja na kujua namna ya kuripoti vitendo vya ukatili ambao waathirika wakuu wametajwa kuwa ni watoto na wanawake.

Awali akitambulisha Kampeni hiyo Bw.Antony Elias kutoka Wizara ya katiba na sheria amesema kuwa serikali ya awamu ya sita imefanya mambo mengi katika nyaja mbalimbali lakini ikaona ni vyema ije na kampeni ya msaada wa kisheria kwa wananchi ambayo itatolewa bure kabisa.

‘’Serikali ya awamu ya sita imefanya mambo mengi lakini ikaona bado kuna changamoto kwenye masuala ya sheria ndio maana ikaamua kuja na kampeni hii maalumu inayohusu masuala ya kisheria’’ alisisitiza Bw Elias.

Aidha Bw . Elias amesema kampeni ya huduma ya msaada wa kisheria ya Mama Samia kwa Wilaya ya Mkalama imelenga kufika katika  Kata 10 na vijiji 30 ambapo amewaomba wananchi wa maeneo husika kujitokeza kwa wingi kupata elimu ya masuala ya kisheria,

Kampeni hii ya huduma ya msaada wa kisheria Kitaifa ilizinduliwa April 27, 2023 ambapo mgeni Rasmi alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Kassim Majaliwa na kwa Mkoa wa Singida imezinduliwa Januari 10 , 2024 na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Pindi Chana na tayari ishafika katika Mikoa sita ikiwepo Dodoma, Manyara, Shinyanga, Ruvuma, Simiyu pamoja na Singida.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.