• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Jukumu la kusimamia miradi ya Maendeleo Wilayani Makalama ni la kila mtu

Imewekwa kwenye: November 30th, 2021

Watendaji wa Serikali katika ngazi ya Kata, Tarafa na vijiji mkoani Singida wametakiwa kutumia muda wao mwingi katika kusimamia ujenzi wa vyumba vya madarasa unao endelea katika maeneo mbalimbali mkoani hapa ili kufanikisha ujenzi huo kwa wakati na kwa viwango vilivyokusudiwa.


Mkoa wa Singida umepokea fedha za UVIKO 19 kiasi cha Sh.Bilioni 13.24 kwa upande wa elimu ili kujenga  vyumba vya madarasa 632 ambapo vyumba 330 ni kwa ajili ya shule za sekondari na 330 shule za msingi pamoja na  mabweni mawili (2) kwa ajili wenye mahitaji maalum ikiwa ni  matarajio ya Serikali kwamba fedha hizo zitasimamiwa na kukamilisha ujenzi huo.


Kauli hiyo imetolewa na  Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko jana tar. 29.11.2021 wakati akikagua miradi mbalimbali ya ujenzi wa vyumba hivyo katika Wilaya ya Mkalama ambapo amebainisha kwamba hali ya ujenzi inaendelea  vizuri na vyumba vingi vimefikia katika hatua ya lenta na vingine vikisubiri kupauliwa.


Aidha katibu Tawala  Mwaluko amewataka viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo watendaji wa vijiji, Kata na Tarafa kuhakikisha haipiti siku bila kujua kinachoendelea katika miradi hiyo ambayo inatakiwa kukamilika kabla ya  tarehe 15 Desemba mwaka huu.


Akiwa katika miradi hiyo Dorothy Mwaluko ametuma  ujumbe kwa wakuu wa shule zote mkoani Singida zenye miradi inayotumia fedha za UVIKO 19 kuhakikisha wanajenga kwa kufuata michoro iliyokubalika na kuhakikisha kwamba wanafanya mawasiliano ya karibu na wahandisi wa Halmashauri za wilaya zao endapo kuna umuhimu wa kufanya hivyo ili kulinda ubora na viwango vilivyotajwa na wataalamu hao.


Katika hatua nyingine amewataka viongozi kuhakikisha wanazishirikisha kamati za ujenzi wa madarasa  na kamati za mapokezi ya vifaa vya ujenzi, kiasi cha fedha zilizokuja na namna ya matumizi ya fedha hizo kama sehemu ya kuweka uwazi na kutengeneza dhana ya  ushirikishwaji.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Sophia Kizigo amesema wilaya imepokea fedha kwa ajili ya ujezi wa vyumba vya madarasa 63 na  ya shule shikizi 16 ambazo kwa jitihada wanazofanya vyote vitakamilika Kwa  wakati.


Aidha Mhe. Kizigo amesema  hali ya ujenzi kwa sasa inaendelea vizuri baada ya kumaliza changamoto ya upatikanaji wa vifaa vya ujenzi ambavyo  vilikuwa havipatikani kwa kuwa zoezi la ujenzi wa vyumba vya madarasa unafanyika nchi nzima hivyo kusababisha changamoto za upatikanaji wa vifaa hivyo.


Amesema kwa sasa Wilaya imeshanunua vifaa vyote vinavyo hitajika katika ujenzi huo ambapo amebainisha kwamba 85% ya majengo yamefikia hatua ya  kufungwa lenta wakati asilimia 15% vinafungwa mkanda wa katikati ili kuondoa nyufa zinazoweza kutokea.


" mbao zitakazotumika kwa wilaya nzima tayari zimeshafika  kilichobaki ni kuzisambaza kwenye shule mbalimbali na mpaka kufikia kesho jioni mabati nayo yatakuwa yamefika". alibainisha Dc Kizigo.


Pia ametuamia fursa hiyo  kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama  Samia Suluhu Hassani kwa kutoa fedha hizi katika Wilaya ya Mkalama jambo ambalo amesema limeondoa kabisachangamoto ya uhaba wa madarasa.


Ziara hiyo imehusisha  viongozi mbalimbali  wa Wilaya ya Mkalama ambapo walitembelea Miradi katika shule ya Ibaga Kata ya Ibaga ambapo kunajengwa vyumba vitano (5) vya madarasa, Shule ya Sekondari Nduguti kunakojengwa vyumba viwili (2), Shule ya Sekondari Gunda Kata ya Ilunda kunakojengwa chumba kimoja, Shule ya Sekondari Grace Mesaki kunakojengwa chumba kimoja, Kikhonda  Sekondari kwenye ujenzi wa vyumba vitatu (3) na Shule ya Sekondari Iguguno kunakojengwa vyumba vine (4) vya madarasa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.