• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Jamii ya Wahadzabe inayoishi Kijiji cha Munguli wakabidhiwa Hati miliki ya Kijiji na Msitu wa asili ya Wahadzabe.

Imewekwa kwenye: November 28th, 2021

Jamii ya Wahadzabe inayoishi Kijiji cha Munguli Kata ya Mwangeza wametakiwa kutumia  hati miliki walizopewa kujiletea maendeleo na kushirikiana katika kutunza  msitu wa Asili wa wahadzabe ili kunufaika na msitu huo unaowapatia Matunda pori, mizizi  ,nyama na asali ambayo ilikuwa shauku yao ya muda mrefu.


Hayo yamesemwa na Diwani kata ya Mwangeza Mhe.Bosco Samweli ambaye pia ni Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya  ya Mkalama wakati akikabidhi hati hizo kwa jamii ya Wahadzabe iliyofanyika katika Kijiji cha Munguli, Kitongoji cha kipamba wilaya ya mkalama.


Aidha Mhe.Bosco amesema kuwa hati hizo zikawe chachu ya wao kulinda Msitu wa asili ambao ulifanyiwa mchakato wa matumizi bora ya ardhi na hatimaye umekamilika hivyo kuwataka kuendeleza ushirikiano wao katika kuulinda na kuheshimu maeneo tengefu ikiwa ni pamoja na maeneo ya makazi, malisho, vyanzo vya maji pamoja na eneo la msitu.


Afisa Ardhi wilaya ya Mkalama Bw.Imikugwe Mwanitu amesema kuwa kupata hati hizo ni kuendelea kutoa  hati za kimila kwa jamii hiyo na kwa mtu mmoja mmoja ambaye anataka ardhi yake ifanyiwe mpango wa matumizi bora  ya Ardhi hivyo kuwataka viongozi wa Kijiji cha Munguli kutunza cheti hicho katika  hali ya usalama kwa manufaa ya kizazi kijacho.


Katika hatua nyingine Afisa Mazingira wilaya ya Mkalama Bw.Amon Sanga amesema  Halmashauri ya wilaya ya Mkalama kwa kushirikiana na timu ya shirika la ujamaa wa jamii katika kulinda raslimali (Ujamaa Community Resource Team)  walianza  mchakato wa kupata hati tangu mwaka 2018/2019 ambapo walianza upimaji wa maeneo yaliyotengwa hadi kukamilisha mchakato wa utoaji wa hati wa Kijiji na Msitu wa Munguli ilikurahisisha upatikanaji  wa hati miliki kwa maeneo mengine katika kutimiza takwa la kisheria.


Naye Afisa Uwanda kutoka  shirika la ujamaa wa  jamii katika kulinda raslimali (UCRT) Bw Julius Mando ameitaka jamii hiyo kutunza msitu wa Asili kwa faida ya jamii na kuhakikisha Ardhi yao inabaki salama na kupata manufaa kama wanavyopata jamii ya wahadzabe inayoishi Mkoa wa Manyara kupitia msitu wao walioingia mkataba na shirika la Carbon Tanzania.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.