• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

DAS MASINDI AONGOZA KIKAO CHA KAMPENI YA CHANJO YA SURUA NA RUBELA WILAYANI MKALAMA

Imewekwa kwenye: February 12th, 2024


Katibu Tawala wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Peter Masindi amewataka wajumbe wa kamati ya Afya Msingi ngazi ya Wilaya (PHC), Wakuu wa idara na vitengo pamoja na Viongozi wa dini Wilaya ya Mkalama kuhakikisha wanawahamasisha wazazi wenye watoto wa umri wa miezi 9 hadi 59 kwenda kwenye vituo vya kutolea huduma za afya Ili waweze kupata chanjo ya Surua na Rubella .


Ameyasema hayo mapema Leo February, 12,2024 wakati akifungua kikao cha maandalizi ya chanjo ya Surua kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mkalama ,ambapo amewataka Kila mmoja kwa nafasi yake kutoa elimu kwa jamii kuwalinda watoto kwakuwapa chanjo Ili kuwakinga na Surua pamoja na Rubela.


Pamoja na hayo Masindi amewataka wataalamu kutumia lugha nzuri kwa Wananchi na kuhakikisha wanakuwa waadilifu katika kazi hiyo kwani inahusu Afya, huku akiwataka kuambatana na viongozi wa Serikali za vijijini na Kata Ili kurahisisha majukumu yao .



"Nendeni mkawatumie viongozi wa vijiji ,kata na vitongoji Ili kufanikisha zoezi letu Ili tuje kujipima tumefikia malengo yetu kwa kiasi gani ‘’ Alisisitiza Das Masindi

Hyasinta Alute Muuguzi Mkuu Mkoa wa Singida, ambaye pia ni mratibu wa chanjo Mkoa aliwataka wataalamu watakaoenda kutoa chanjo kuhakikisha watoto wote wenye umri wa kupata chanjo wanapatiwa ili kuwakinga na ugonjwa wa Surua ambao uliotajwa kuwepo mwaka jana katika Kata ya Mwangeza na kuwasihi kufanya kazi kwa moyo na bidii kuhakikisha wanawafikia watoto wapatao elfu 34 ndani ya Wilaya ya Mkalama.


Awali akiwasilisha taarifa , Mratibu wa chanjo Wilaya ya Mkalama Tope Webiro amesema kuwa Wilaya inakusudia kuchanja Zaidi ya Watoto elfu 34 kwenye maeneo mbalimbali ikiwepo Shule, Vituo vya kutolea huduma za Afya, Masoko , Vituo vya basi(Stendi) ambapo amesema kutakuwa na vituo 38 vya kudumu pamoja na vituo 17 vya kuhama hama hivyo kutoa wito kwa wazazi kupokea chanjo hiyo kwa mtazamo chanya ili kuwalinda watoto dhidi ya Surua na Rubela.



Chanjo hii inatarajiwa kuanza February 15-18 kwa Nchi nzima ikiwa na kauli mbiu isemayo ‘’ONYESHA UPENDO MPELEKE MTOTO AKAPATE CHANJO’’


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.