• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Daraja hili ni kivutio Mkalama- Masaka

Imewekwa kwenye: March 2nd, 2018

Takribani shilingi Bilioni moja zimeokolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kwa kushirikiana na Wakala wa barabara mijini na vijijini (TARURA) baada ya kukamilisha daraja la kisasa kabisa la waenda kwa miguu na vyombo vingine vya usafiri lililopo katika kijiji cha Msingi kwa kiasi cha Shilingi milioni 300,007,920.00

Usanifu uliofanywa awali na makisio ya gharama za ujenzi wa daraja hilo kwa kutumia teknolojia iliyozoeleka ya zege na nondo unaonesha daraja hilo lilipaswa kugharimu kiasi cha Shilingi bilioni 1,300,000,000.00 lakini baada ya kubaini uwepo wa rasilimali za kutosha za mawe na mchanga, Halmashauri iliamua kujenga daraja hilo kwa kutumia rasilimali hizo tu jambo lililoifanya Mkalama kuwa ya pili kuwa na daraja la aina hiyo baada ya lile lililopo Wilayani Ludewa.

Daraja hilo lililojengwa kwa teknolojia ya Mawe na Mchanga tu lina urefu wa mita 45 huku likiwa na matundu makubwa manne ya kupitishia maji na lina uwezo wa kupitisha mzigo usiozidi tani 10.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi daraja hilo kwa wananchi wa Kata ya Msingi na wanufaika wengine wa daraja hilo ambao kwa pamoja waliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka, meneja wa TARURA wilayani hapa Mhandisi Ephraim Kalunde alisema kuwa mkataba wa ujenzi wa daraja hilo ulijumuisha pia kazi ya ufunguaji wa barabara yenye urefu wa mita 605 kwa ajili ya mapokeo ya daraja.

“Mhe. Mkuu wa Wilaya, TARURA ambao ndio wasanifu na wasimamizi wa mradi huu wameweza kutumia na kuitambulisha teknolojia ya ujenzi wa madaraja na miundombinu ya barabara kwa kutumia Mawe ambayo mbali na kuwa imara zaidi, teknolojia hii ni nafuu ukilinganisha na teknolojia nyingine kama ile ya kutumia zege na nondo nyingi” Aliongeza Mhandisi Kalunde.

Mara baada ya kukabidhiwa daraja hilo kwa niaba ya wananchi, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka ameipongeza timu yote iliyofanikisha kukamilika kwa ujenzi wa daraja hilo huku akiwataka wananchi kutunza na kulinda mradi huo kwa kutokata miti iliyopo kwenye mto unaopita chini ya daraja na kutochimba mchanga karibu na daraja hilo.

“Mbali na kuwa kivuko kwa watembea kwa miguu na vyombo vya usafiri, daraja hili ni kivutio kikubwa sana cha wageni mbalimbali waliopo nje ya Mkalama na kuna watu wengi sana kutoka sehemu mbalimbali watakuja kuona na kujifunza teknolojia hii mpya ya viwango vya hali ya juu kabisa” Alisema Mhe. Masaka.

Mhe. Masaka pia aliwataka wananchi wanaoishi kando ya daraja hilo kutumia fursa ya uwepo wa kivuko hicho kuongeza kiwango cha uzalishaji wa mazao mbalimbali ya biashara ili daraja hilo liwe na tija ya kusafirisha mazao hayo badala ya kulitumia kupigia picha tu.

“Daraja hili ni muendelezo wa mambo mazuri yanayoendelea kufanywa na serikali ndani ya Wilaya ya Mkalama na muda si mrefu sana barabara ya kutoka Bariadi mkoani Simiyu mpaka Iguguno Mkoani Singida kupitia daraja la Sibiti itajengwa kwa kiwango cha lami na tayari serikali imeanza kutafuta fedha za kutekelezea mradi huo hivyo ndani ya kipindi cha miaka hii mitano, Mkalama itakuwa na Maendeleo makubwa sana.

Ujenzi wa daraja hilo umetumia muda wa Miezi 7 mpaka kukamilika kwake ikiwa ni nyongeza ya mwezi mmoja zaidi baada ya kuwepo kwa kazi za nyongeza ambazo hazikuwepo kwenye usanifu wa awali ambapo ulianza tarehe 07/07/2017 na umekamilika tarehe 16/02/2018.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YAKABIDHI KADI ZA MATIBABU BURE KWA WAZEE MKALAMA

    June 15, 2025
  • SIKU YA MTOTO WA AFRIKA WILAYANI MKALAMA

    June 16, 2025
  • Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkalama Apongeza Ujenzi wa Zahanati ya Nkenke

    June 13, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA SIASA MKOA WA SINGIDA

    June 11, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.