• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI MKALAMA LAFANYIKA

Imewekwa kwenye: November 15th, 2017

Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama limefanyika leo huku hoja mbalimbali zikiibuliwa na kupatiwa majibu.

Baraza hilo ambalo ni la kwanza kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 liliipa kipaumbele sekta ya Elimu na Kilimo ambapo madiwani walielezea hali ya utekelezaji katika sekta hizo na changamoto zinazopatikana  kutoka kwenye kata zao huku pia wakiainisha mikakati mbalimbali waliyojiwekea kukabiliana na changamoto hizo.

Moja ya hoja zilizoibuliwa katika baraza la leo ni changamoto zilizojitokeza katika zoezi la uandikishaji wa vitambulisho vya Taifa ambapo katika baadhi ya vijiji mashine zimeshindwa kusoma alama za vidole za baadhi ya wananchi waliojitokeza kujiandikisha.

Akijibu juu ya hoja hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mhandisi Godfrey Sanga amekiri kupokea taarifa za kuwepo kwa changamoto hiyo ambapo amewatoa hofu wananchi hao kwa sababu mamlaka husika  inaendelea kushughulikia suala hilo na pindi likipatiwa ufumbuzi wananchi hao wataarifiwa.

Diwani wa Kata ya Ilunda Mhe. Mohamedi Imbele alitaka kujua mipango na mikakati ambayo Halmashauri imeweka ili kuhakikisha kunakuwepo na maadhimisho ya Wilaya ya Sikukuu ya Wakulima na Wafugaji  maarufu kama Nane Nane ambapo Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira Mhe. Erasto Linza alimhakikishia Mhe. Imbele na Wananchi wote wa Wilaya ya Mkalama kuwa mipango ya kuhakikisha sikukuu hiyo inaadhimishwa ngazi ya Wilaya inaendelea vizuri na hatua iliyobaki ni kupanga Sehemu ambayo maadhimisho hayo yatafanyika kwa Mwaka ujao.

Suala la utunzaji wa vyanzo vya maji lilikuwa ni moja ya mambo yaliyoibuliwa katika baraza hilo ambapo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mhe. James Mkwega alitoa msimamo wa Halmashauri ya Wilaya kuwa kuanzia sasa gharama za kurejesha huduma ya maji katika  kijiji ambacho watu wake watahujumu vyanzo na miundombinu ya Maji zitatolewa na kijiji husika na si halmashauri.

Baraza hilo hutanguliwa na baraza la Kata ambapo waheshimiwa madiwani hupokea majibu ya wataalam kuhusu changamoto mbalimbali zilizopo kwenye kata zao na kuziwasilisha kwa wataalam kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.