• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI LACHUKUA HATUA ZA KINIDHAMU KWA WATUMISHI WATATU WILAYANI MKALAMA

Imewekwa kwenye: March 16th, 2023


Baraza la Madiwani limefanya, maamuzi ya kumfukuza kazi Mtumishi mmoja, limetoa Onyo kwa kwa Mtumishi mmoja na kumshusha Cheo Mtumishi mmoja baada ya kupitia mashauri ya kinidhamu kwa watumishi hao watatu.

Maamuzi hayo yamefanyika katika Mkutano wa Halmashauri wa robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2022-2023 uliofanyika  leo Machi 16, 2023, ambao ulipitia na kujadili taarifa za robo ya pili ambazo ziliwasilishwa na Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Halmashauri.


Pamoja na kupitia na kujadili taarifa za utekelezaji wa shughuli za Serikali za robo ya pili Mkutano wa Halmashauri ulihitimisha mashauri ya kinidhamu  na kufanya maamuzi ya kumfukuza Mtumishi mmoja, limetoa Onyo kwa Mtumishi mmoja na kumshusha cheo Mtumishi mmoja.


Akiwasilisha maamuzi ya Kamati ya Baraza zima ambalo lilijigeuza kama Kamati Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mhe. James  Mkwega ameeleza kuwa


 “waheshimiwa wajumbe tuliwaomba mtupishe kwa muda ili Baraza lijigeuza kuwa Kamati ya Utumishi na hapa tulikutana na mashitaka matatu ya Watumishi, Mtumishi wa kwanza ni Mtendaji wa Kijiji cha Kidarafa lakini siyo huyu aliyepo sasa nisahihishe kabisa. Baraza baada ya kukaa na kuchunguza na kujiridhisha tuhuma zake na utetezi alioutoa kwenye Kamati ya Fedha imetoa maamuzi yafuatayo; Baraza limemuamuru kurudisha kiasi cha Shilingi 601,000/= alizozitumia huyu Mtendaji kinyume na utaratibu ndani ya miezi mitatu na kupewa Onyo. Mtumishi wa pili tumesikiliza tuhuma za Afisa Elimu vielelezo baada ya kujiridhisha kama Baraza, Baraza limeamua kumshusha cheo na kuamua abadilishiwe kituo cha kazi wakati akiwa kwenye muda wa matazamio. Shitaka la tatu, Baraza limejiridhisha kwa kina juu ya Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Maziliga na kufanya maamuzi yafuatayo; Baraza limeamua kutoa adhabu ya juu kabisa kwa Mtendaji huyu baada ya kujiridhisha na kuona tuhuma zake alizotuhumiwa ni nzito lakini bado hakuonyesha mabadiliko ya tuhuma hizi baada ya kukutana na Kamati ya Fedha kwa hiyo Baraza limemfukuza kazi Mtendaji huyu kwa kushindwa kusimamia majukumu yake”  Aliongeza Mhe. Mkwega


Pamoja na hayo Mhe. Mkwega amewataka watumishi kuwa waadilifu na kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria na Taratibu za kazi ili kuepuka hatua za kinidhamu zinazoweza kuchukuliwa dhidi yao .


Aidha, aliongeza kwa kuwataka watumishi kuwa na ratiba nzuri za kazi zao na kuacha kusubiri Maazimio ndipo waanze kutekeleza wajibu wao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.