• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

BAJETI YA MWAKA 2023/2024 IMEZINGATIA VIPAUMBELE MUHIMU

Imewekwa kwenye: January 27th, 2023


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mhe. James Mkwega amempongeza Mkurugenzi Mtendaji na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kwa kuandaa bajeti nzuri   iliyozingatia vipaumbele mbalimbali iliyojikita kwenye miradi ya

 maendeleo ya wananchi inayoakisi uhalisia.


Ametoa pongezi hizo mapema leo  January 27, 2023 wakati akifungua kikao maalumu cha Baraza la Madiwani la  kupitia na kujadili mapendekezo ya bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka wa  fedha 2023/2024.

‘’ kwa kweli ninakupongeza Mkurugenzi Mtendaji na timu yako mmeandaa bajeti nzuri inayozingatia vipaumbele na mahitaji ya Halmashauri na kwa namna bajeti hii ilivyo ina kwenda kuleta mahitaji ya maendeleo ya  Wanamkalama’’aliongeza Mhe. Mkwega.


Pamoja na Bajeti hiyo nzuri Mhe. Mkwega alisema kuna maeneo amabayo hayajapangiwa bajeti kama vile kukarabati maboma yaliyochakaa na barabara hivyo aliwaomba wanaohusika kuangalia kwa jicho la Tatu ili maeneo hayo yatengewe bajeti.


Mhe. Mkwega  aliwatia moyo watumishi kila mmoja kwa nafasi yake kufanya kazi kwa bidii huku wakiendelea kudumisha upendo na ushirikiano ili kuchochea maendeleo ya Halmashauri, huku akiwataka kusimamia vyema miradi inayotolewa na Serikali na hatimaye kukamilika kwa wakati.

Sanjari na hayo Mhe. Mkwega alimtaka Mkurugenzi kupitia Ofisi ya Mipango kuandaa taarifa ya utekelezaji kwa kila kata zenye miradi na kuzisambaza kwa Madiwani , kubainisha thamani ya mradi na utekelezaji wake ni kwa muda gani.


 Awali akisoma  Rasimu ya Mpango wa bajeti  Kaimu Afisa Mipango Bw. Daniel Tesha alisema kuwa kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama imejipanga kukusanya na kutumia jumla ya Shilingi 27 ,073,624,492.00 kwa ajili ya Mishahara na Matumizi Mengineyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mkalama, Mhe. Lameck Itungi alisema kuwa kazi ya Chama cha Mapinduzi ni kuhakikisha  inasimamia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani na kuwataka Madiwani kwenye Mikutano yao kusema mazuri yaliyofanywa na  Serikali ya awamu ya Sita.


‘’Ifike wakati sasa Waheshimiwa Madiwani muhubiri maendeleo yaliyofanywa na serikali ya awamu ya sita kwenye Kata zenu  kuwaambia wananchi mazuri yanayofanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi’’ Aliongeza Bw. Itungi

Akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi , Afisa Elimu Sekondari  Mwl . Said Kalima amesema atahakikisha bajeti hii inasimamiwa kwa weledi mkubwa kama ilivyokuwa kwa bajeti iliyopita na kuhakikisha wanaongeza makusanyo ya Halmashauri  na kuvuka lengo na kuongeza kuwa watashirikiana na Wataalamu wake kusimamia  fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo  zinafanya kazi iliyokusudiwa na kukamilika kwa wakati.

Matangazo

  • Uzinduzi wa Msimu mpya wa Kilimo kufanyika October 20 2021 October 18, 2021
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI YENYE MAREKEBISHO June 29, 2022
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI YENYE MAREKEBISHO June 29, 2022
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI YENYE MAREKEBISHO June 29, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI LACHUKUA HATUA ZA KINIDHAMU KWA WATUMISHI WATATU WILAYANI MKALAMA

    March 16, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI LACHUKUA HATUA ZA KINIDHAMU KWA WATUMISHI WATATU WILAYANI MKALAMA

    March 16, 2023
  • JAMII HAKIKISHENI MNAKOMESHA UKATILI

    March 08, 2023
  • ZIARA YA KATIBU MKUU CCM KULETA NEEMA YA VITUO VYA AFYA WILAYANI MKALAMA

    March 02, 2023
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    MKALAMA DISTRICT COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi: +255 758 954 045

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.