• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Wilaya ya Mkalama ipo Imara katika suala la Amani na utulivu

Imewekwa kwenye: May 11th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Mkalama Mhe.Sophia Kizigo amesema Serikali wilayani hapa imejipanga kikamilifu kuhakikisha Wilaya inakua katika hali ya amani na utulivu na kuwaonya wote watakaojaribu kuvunja sheria hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.


Ameyasema hayo Leo wakati akitoa salamu za Serikali katika kikao Cha baraza la kawaida la madiwani robo ya tatu (3).


Pamoja na salamu hizo amewataka madiwani pamoja na viongozi wa Serikali na dini kuhamasisha Wananchi juu ya ushiriki  wa zoezi la Sensa ya watu na Makazi inayotarajiwa kufanyika Agosti 23 Mwaka huu na kuwa zoezi hilo litasaidia  Serikali kupanga bajeti kulingana na idadi sahihi ya watu pamoja na vipaumbele vilivyopo katika jamii.


Aidha Kizigo ameendelea kusisitiza kuwa Serikali itasimamia agizo lake la kupiga marufuku waganga wa tiba za asili (Lambalamba) ambao wamekuwa wakileta taharuki Kwa jamii kutokana na kupiga ramli chonganishi jambo ambalo halikubaliki.


"Tayari kuna watu waliokuwa wakijuhusisha na vitendo hivyo tumekwisha wakamata na wengine wataongezeka baada ya upelelezi kukamilika hivyo napenda kutoa onyo kwa mara nyingine kwa wale tutakao wabaini wakifanya hivyo tutaendelea kuwakamata" alisema Kizigo.


Akisisitiza umuhimu wa Sensa kitaifa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama James Mkwega alisema ni vema zoezi hilo liwafikie wananchi wa kabila la Waazabe ambao maisha yao nitofauti na watu wengine kimazingira.


Amesema kundi hilo la wananchi linapaswa kupewa elimu ya sensa ya mara Kwa mara Ili walielewe na kujitokeza Kwa wingi katika zoezi hilo ambapo Mratibu wa Sensa wilayani hapa  Bw. Daniel Tesha alisema tayari mazingira mazuri yameandaliwa dhidi yao.


 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mkalama Bi. Asia Messos ametaja shughuli zinazoendelea wilayani hapa kuwa ni pamoja na zoezi la Anuani za Makazi na Postikodi ambapo amewaomba madiwani kuhakikisha wanasimamia zoezi hilo vizuri Ili Kila nyumba kuwa na namba.


Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki Mhe. Francis Isack Mtinga amesema kwasasa bunge la bajeti linaendelea na akiwa kana mwakilishi wa Wananchi anahakikisha wanaomba bajeti kubwa ya fedha Ili kutekeleza miradi ya maendeleo.


Aidha ameiomba Halmashauri  kujenga soko la kawaida na vitunguu Ili kuinua Uchumi wa Wilaya ya Mkalama.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.