• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU KOMESHENI RUSHWA YA NGONO KAZINI

Imewekwa kwenye: May 1st, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba,ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani kwa kushirikiana na vyama vya wafanyakazi kuhakikisha rushwa  ya ngono na unyanyasaji wa kijinsia  inatokomezwa katika mkoa huu.


Akizungumza leo (Mei Mosi) 2023 wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya wafanyakazi  kimkoa zilizofanyika Manispaa ya Singida, amesema tatizo la rushwa ya ngono ni lazima likomeshwe kwenye Mkoa wa Singida.


Serukamba ameliagiza Shirika la Bima mkoa wa Singida kufanya uhakiki wa wafanyakazi ambao Bima zao zimeiva waweze kulipwa na Wakurugenzi wa Halmashauri ambao hawajawalipa watendaji posho za kila mwezi kuanza kulipa  posho watendaji wa kata  ndani ya miezi mitatu na kutoa taarifa kwake.


"Nichukue nafasi hii kumpongeza Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa kuwapandisha madaraja watumishi waliokuwa wanastahili hali ambayo imeleta motisha na tija katika utendaji kazi kwa watumishi ," alisema Serukamba.


Naye Mratibu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Mkoa wa Singida,Maria Bange, akisoma risala ya wafanyakazi amesema rushwa ya ngono katika harakati za kutafuta ajira imepungua katika kipindi cha 2022/2023.


Amesema katika kipindi hicho kumekuwa na changamoto kadhaa ikiwamo baadhi ya viongozi kuwaweka ndani wafanyakazi bila Kufuatia utaratibu na sheria za Kazi.


Ameongeza kuwa changamoto nyingine ni nyongeza ya mishahara iliyofanyika mwaka jana haijakidhi matarajio ya wafanyakazi, kutolipwa kwa wakati fedha za Uhamiaji,likizo na malimbikizo ya mishahara kucheleweshwa hadi wengine kustaafu na ucheleweshaji wa pesheni kwa wastaafu.


Ameendelea kutaja Changamoto nyingine kuwa  Shirika la Bima kutowalipa watumishi waliokata Bima ya maisha wakati Bima zao zinapoiva,waajiri binafsi kutowasilisha Makato ya asilimia 10 kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii,waajiri kutopeleka michango ya hifadhi ya jamii kwa wakati na kusababisha tozo kubwa.


Bange amesema pamoja na changamoto hizo  wafanyakazi wanaomba serikali iongeze nyongeza ya kima Cha chini Cha mshahara inayoendana na hali ya uchumi wa sasa,kuhamisha wafanyakazi kuendane na ulipaji wa stahiki zao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YAKABIDHI KADI ZA MATIBABU BURE KWA WAZEE MKALAMA

    June 15, 2025
  • SIKU YA MTOTO WA AFRIKA WILAYANI MKALAMA

    June 16, 2025
  • Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkalama Apongeza Ujenzi wa Zahanati ya Nkenke

    June 13, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA SIASA MKOA WA SINGIDA

    June 11, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.