• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MSITU WA MUNGULI KUTANGAZWA KATIKA GAZETI LA SERIKALI

Imewekwa kwenye: January 6th, 2023


Wakazi wa Kijiji cha Munguli kilichopo Kata ya Mwangeza Wilayani Mkalama wameridhia  kutangazwa kwa hifadhi ya  Msitu  wa Munguli  wenye ukubwa  wa  Hekta 1656, katika Gazeti la Serikali ili kuhakikisha Msitu huo unalindwa na kutunzwa ili uweze kuwapatia manufaa.


Wamefanya maridhiano hayo January 5, 2023 katika mkutano Mkuu wa Kijiji uliofanyika katika Kijiji cha Munguli Kata ya Mwangeza.


 Afisa Maliasili  Mkoa wa Singida Bw. Charles Kidua aliwaeleza wananchi umuhimu wa  kutangazwa kwa Msitu huo katika Gazeti la Serikali  kuwa utawapa manufaa makubwa kwani ngazi za juu  zitautambua Msitu  pamoja na kuwekwa kwa Sheria ndogo  za  Usimamizi Shirikishi wa Msitu na kupelekea  watakao haribu kwa makusudi bila kufuata taratibu kuchukuliwa hatua.


Aidha, Bw. Kidua alitaja  faida za utunzaji wa Msitu kuwa ni kupata fedha kwa kunyonya hewa ya ukaa hivyo kupunguza kero ya kutoa michango ya maendeleo mara kwa mara pindi inapojitokeza.


‘’ katika kupambana na mabadiliko ya  tabia  Nchi  kama ilivyokuwa zamani lazima kila mtu ajue umuhimu wa hifadhi ya mazingira na utunzaji wa msitu ambao hivi karibu utatangazwa katika gazeti la  Serikali  ili Wananchi wa Munguli waweze  kunufaika na Msitu huu kama ilivyo kwa jamii ya Wahadzabe waliopo Yaeda chini Mkoani Manyara’’ aliongeza Bw. Kidua.


 Mwanasheria wa Wilaya ya Mkalama Bw, Daud Makendi aliwataka wananchi kufuata Sheria na taratibu ili kuepuka kuingia katika makosa  ya kisheria ikiwa ni pamoja na kutoa katazo la kuingia na kufanya shughuli zozote za kibinadamu ndani ya msitu bila kupata kibali cha maandishi  kutoka kwa Mamlaka husika.


Aidha, Bw. Makendi aliongeza kuwa mtu yeyote atakayekiuka au kwenda kinyume na kifungu chochote cha sheria ndogo  atakuwa ametenda kosa na akipatikana na hatia atatozwa  faini isiyopungua shilingi elfu Hamsini  na isiyozidi Laki moja  ikiwa ni pamoja na kulipa fidia ya uharibifu  baada ya tathimini kufanyika au kifungo kisichopungua miezi sita na kisichozidi miezi kumi na mbili au vyote faini na kifungo kwa pamoja.


Baadhi ya wananchi waliokuwa kwenye Mkutano huo waliahidi kuulinda na kutunza  hifadhi ya Msitu bila kuvunja Sheria ndogo  na kuridhia kwa pamoja kuwa msitu wao utangazwe kwenye gazeti la serikali .

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.