• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Jamii imetakiwa kutoa ushirikiano na kufichua vitendo vya Ukatili Kwa Watoto.

Imewekwa kwenye: June 17th, 2022

Jamii imetakiwa kupinga vitendo vya ukatili kwa watoto  na kuripoti vitendo hivyo kwenye vyombo vya sheria  na kutoa  ushahidi  kwa vyombo  hivyo  ili kusaidia  kuchukuliwa  hatua stahiki kwa wanaoendelea kufanya vitendo hivyo.


Kauli  hiyo imetolewa juni 16 na Remigius Ngole  Afisa  Tarafa,  Tarafa ya Nduguti alipomwakilisha  Mkuu wa Wilaya  ya Mkalama  katika kilele cha siku ya mtoto wa Afrika  kilichofanyika katika kijiji cha Iambi Kata ya Ilunda  Wilayani hapa.


‘’Bado vitendo vya ukatili kwa watoto  vinatishia  ustawi kwa watoto  wetu, vitendo vya kupigwa , kubakwa , kulawitiwa pamoja na mimba  kwa wanafunzi havikubaliki katika jamii, hivyo naagiza vyombo vya dola kuchukua  hatua stahiki  kwa wote  wanaofanya vitendo hivi kwa watoto, hivyo ninatoa  rai kwa wananchi kufichua vitendo hivi’’. Aliongeza Ngole.


Ngole aliongeza kuwa migogoro ya ndoa imekua ni chanzo cha watoto kufanyiwa ukatili na kuzalisha tatizo la ongezeko la watoto wa mitaani  kwani wanakosa  haki za msingi kwakukosa malezi mazuri ya wazazi  pamoja na kukosa haki ya kupata elimu hivyo kuwataka wazazi kuepuka migogoro hiyo kwa ustawi wa watoto kwani ni taifa la kesho.


Aidha aliongeza kuwa serikali ya awamu ya Sita imekua ikifanya jitihada za kuhakikisha watoto wanakua kwenye mazingira mazuri  na kupata elimu  bora na kwakujali hilo imetenga fedha  shilling 96,200,000 kwaajili ya ujenzi wa bweni la wasichana shule ya sekondari  Malaja  ili  kupunguza vishawishi kwa watoto wa kike na kutimiza malengo yao .


Awali akimkaribisha Mgeni  rasmi Afisa  Maendeleo Wilaya ya Mkalama Mohamed  Atiki alisema siku ya mtoto wa Afrika huazimishwa kila ifikapo june 16 kila mwaka  na Nchi 51 wanachama wa Umoja  wa Nchi huru za Afrika(O.A.U).


Atiki aliongeza kuwa lengo la maadhimisho haya ni kukumbuka  mauaji ya kinyama waliofanyiwa watoto wa  Kitongoji cha Soweto Nchini Afrika Kusini  mwaka 1976 hukuTanzania nayo ikiwa kama mwanachama  wa Umoja  wa Nchi huru  za Afrika  ilianza kuadhimisha siku ya mtoto wa Afrika mwaka 1991.


Wakisoma risala kwa mgeni Rasmi watoto wa  kijiji cha Iambi  walianza kwakuishukuru serikali ya awamu ya Sita kuendelea kutoa elimu bila malipo kuanzia Chekechea hadi kidato cha Nne  na kuongeza kuwa kwa kipindi cha mwaka Mmoja wameshuhudia  juhudi za serikali  katika ujenzi wa madarasa kwa kutumia  fedha za UVIKO 19  jumla ya madarsa 63 yamejengwa  ikiwa kwa shule za  Msingi ni madarasa 16 na  Shule za Sekondari  47 yaliyogharimu shilingi  940,000,000.


Aidha walisema kuwa pamoja na pongezi hizo wamekua wakikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa matukio ya kufanyiwa ukatili huku  wakiomba jeshi la polisi kukamilisha kesi  10 zilizopo kwenye upelelezi pamoja  nakuiomba serikali kuhamasisha wazazi kuchangia chakula shuleni  kwani inapelekea mahudhurio yao  kuwa mabovu pamoja na ufaulu kuwa duni.


Maadhimisho haya huambatana na kauli mbiu mbalimbali ambapo kwa mwaka huu inasema “TUIMARISHE ULINZI WA WATOTO ,TOKOMEZA UKATILI DHIDI YAKE JIANDAE KUHESABIWA’’

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.