• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

HAKIKISHENI MNATOA ELIMU YA LISHE KWA JAMII ' DC MOSES MACHALI '

Imewekwa kwenye: February 8th, 2024


Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Moses Machali amewataka watendaji wa Kata, watumishi wa afya pamoja na wahudumu ngazi ya jamii kuhakikisha wanatoa elimu kwa jamii kuhusu masuala ya Lishe na tamko la jiongeze tuwavushe salama pamoja bima ya afya iliyo boreshwa (iCHF) ili kuhakikisha viashiriavyote vinapata rangi ya kijani na kutoka kwenye rangi ya njano na nyekundu ili kupelekea Wilaya  kuwa katika nafasi nzuri ya Lishe ndani ya Mkoa wa Singida.

Amesema hayo mapema leo February 8, 2024 kati ka kikao cha tathimini ya Lishe kwa kipindi cha robo ya pili  ya mwaka wafedha 2023/2024 kilichofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa  Wilaya ya Mkalama.



Aidha amewataka kila mmoja kwa nafasi yake kutimiza wajibu wake  kikamilifu katika kutoa elimu  ya lishe kwa jamii pamoja na kutembelea watoto chini ya miaka mitano, wamamawajawazito , elimu ya uzazi wa mpango pamoja nakuwaelimisha wazazi kuhusu kuendelea kuchangia chakula shuleni ili  kutengeneza taifa la watoto  wenye  afya bora na wenye utimamu wa akili.


‘’Jitumeni, tusifanye kazi kwa kuvutana suala la lishe ni ajenda ya taifa hakikisheni mnaenda kutoa elimu kwa wananchi iliwaweze kufahamu suala la lishe sahihi , tamko la jiongezetuwavushe salama pamoja na bima ya afya iliyoboreshwa’’ Alisisitiza  Dc Machali.



Pamoja na hayo amewaagiza kuhakikisha wanasimamia vizuri mapato ya Hospitali, Vituo vya afya na zahanati na kuwataka kujenga  utamaduni wa kutembelea Hospitali kujua idadi ya wagonjwa waliopatiwa huduma katika vituo vinavyohusika ili pesa inayopatikana kutokana na matibabu hayo  ziweze kutatua changamoto mbalimbali zilizopo kulingana na ufinyu wa bajeti.



Awali akiwasilisha taarifa ya hali ya Lishe Wilaya ya Mkalama Afisa Lishe Wilaya ya Mkalama Zacharia Nyahende amesema kuwa kama Halmashauri imejiwekea vipaumbele kwa mwaka2023/ 2024 kuwa ni kuhakikisha kitengo cha lishe kinaendelea kuimarisha huduma za lishe hususani kwa watoto chini ya miaka mitano, vijana barehe, wanawake wenye umri wa kuzaa pamoja na wazee huku wakiendelea kupunguza tatizo la virutubisho vya vitamini na madini kwa kuhamasisha shule kutumia unga wa mahindi uliongezwa virutubisho.


Mratibu wa Afya ya uzazi na Mtoto Emmanuel Ngeleja amesema kuwa Wilaya inaendelea kuimarisha mfumo wa M-Mama katika maeneo yote ndani ya wilaya  ili kumsaidia mama na mtoto  na kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuchukua hatua za mapema kwa mama anapojisihi uchungu hasa akiwa nyumbani, kuunda kamati zinazohusika kufuatilia wajawazito pamoja na kuendelea kuhimiza wakinamama kupata huduma ya Utrasound kwa kipindi cha ujauzito  ili kubaini changamoto mapema na kuzifanyia kazi.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.