• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Jamii ya wahadzabe iliyopo Wilayani Mkalama yahesabiwa baada ya kupatiwa kitoeo Cha Nyama

Imewekwa kwenye: August 23rd, 2022


Mkuu Wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Sophia Kizigo amewataka  wananchi wilayani hapa   kuendelea  kutoa taarifa zote sahihi zikiwemo za watu wenye makundi maalum ili kufanikisha zoezi la sensa linaloendelea nchini.


DC Kizigo amesema hayo Leo agosti 23 baada ya kuhesabiwa akiwa nyumbani kwake ambapo amesema zoezi la sensa katika Wilaya  limeenda vizuri.


"Zoezi la sensa katika Wilaya yetu limeenda vizuri sana, tumeanza saa 6 usiku Wa kumkia Leo tarehe 23 tumehesabu watu Wa makundi maalum wakiwemo Mahabusu,watoto Wa mtaani, wagonjwa hospitalini na familia mbalimbali tunawashukuru makarani wetu kwa kufanya kazi nzuri na tunawaomba waendelee mpaka zoezi Litakapokamilika" Alisema Dc Kizigo.


DC Kizigo amesisitiza kwa kuzitaka  familia ambazo  hazijafikiwa na makarani siku ya Leo kutunza taarifa zao sahihi ili makarani watakapo wafikia waweze kufanikisha zoezi hilo Kwa urahisi .


"Nitoe wito kwa wananchi wote ambao hawatafikiwa na makarani Leo basi watunze taarifa zao ili kukamilisha zoezi hili muhimu kwa ustawi wa taifa letu". Alisema DC Kizigo.


Mkurugenzi Mtendaji Wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama  Bi. Asia  Mesoss amesema zoezi la kuhesabu familia ya jamii ya Wahadzabe limefanikiwa kwa asilimia mia moja Mara baada ya kutenga bajeti ya kuwatafutia nyama jamii hio  inayoishi kwa  kwakutegemea shughuli za uwindaji , kula asali ,matunda pori pamoja na mizizi  .


" Tunashukuru tumefika katika kitongoji hiki cha Kipamba hapa Mkalama, kuangalia zoezi hili la sensa linavyoenda tuliona kuwa jamii hiii inategemea sana nyama na asali tukaona tutenge bajeti ambapo tumewapatia ng'ombe na wamehesabiwa kisha wakala nyama zoezi limefanikiwa kwa aslimia 100%." Alisema Mkurugenzi  Asia Messos .


Alisema jamii hiyo ya Wahadzabe inaishi kwa kutegemea uwindaji na asali  mizizi na matunda pori hivyo waliamua kuwapatia nyama ili wabaki kuhesabiwa majumbani mwao.


"Jamii hii inajihusisha na uwindaji  ni watu ambao hawatunzi chakula wala  hawalimi kwahiyo tumeona tulete nyama ambayo ndio chakula chao ili kufanikisha zoezi hili muhimu kwa ustawi Wa serikali yetu". Aliongeza Bi Messos .


Baadhi ya wananchi ambao ni jamii ya Wadzabe wameshukuru serikali ya Halmashauri ya  Wilaya  ya mkalama kwa kuwafanyia zoezi la sensa  pamoja na kuwapatia nyama na kuiomba serikali kuwasaidia kulinda utamaduni wao pamoja na kuwapatia huduma za kijamii .

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.