• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

"HATUWEZI KUPATA MAANDELEO KAMA HATUFANYI KAZI" DC MACHALI

Imewekwa kwenye: December 9th, 2023


Wilaya ya Mkalama imeungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Watanzania wote kuadhimisha miaka 62 ya Uhuru wa Tanganyika kwa kufanya shughuli mbalimbali za Maendeleo Wilayani hapa kwa kupambana miti takribani 700 katika kituo cha Polisi Cha Wilaya pamoja na Hospital ya Wilaya ya Mkalama.

                                                                                                                                    DC Moses Machali

Akizungumza mara baada ya kuhitimisha zoezi la upandaji miti katika kuadhimisha miaka 62 ya Uhuru ambayo huadhimishwa kila Disemba 9 ya kila mwaka, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Moses Machali amewataka wananchi pamoja na watumishi kuwa wazalendo kwa Nchi  kwa kujituma na kuwajibika kwa taifa lao kwakufanya kazi kwa bidii kwaajili ya masilahi mapana ya Nchi yao.

                                                                                                                                    DAS Peter Masindi

“Hatuwezi kupata maendeleo kama hatufanyi kazi, juzi mkuu wa mkoa ametuelekeza njia pekee ya kuhakikisha tunapata maendeleo ni kwa kufanya kazi, Kila kaya inakuwa na angalau hekari mbili, katika msingi huo tunaweza kuleta mabadiliko ambayo tunahitaji”, Mhe. Machali

“Mtumishi wa serikali, mtumishi katika 'private sector' unapokuwa unafanya kazi je, masaa yote ambayo umepangiwa kufanya kazi unayatumia vizuri kuweza kuzalisha kwa ajili ya taifa lako? Watu tumepata Uhuru lakini tunauchezea, watu wanafanya uhuni mahali pakazi.Tubadili tabia zetu, tuwajibike ili tuweze kusukuma maendeleo ya taifa letu”. Alisisitiza Machali

Naye katibu tawala wa Wilaya ya Mkalama,  Peter Masindi amewataka wakazi wa watanzania kuendelea kudumisha amani iliyopo Nchini sambamba na kuendelea kuienzi siku hii muhimu ya Uhuru kwa watanzania kuwakumbuka wazee, viongozi waliojitolea kwa ajili ya Uhuru wa taifa la Tananyika

"Tumefanya hili tukio kwa ajili ya kukumbushana kwamba tuliumia, waliumia na sisi tuumie kwa ajili ya wengine,tusiache hii tarehe ikapita kama ilivyokuja, tarehe itabadilika, lakini maendeleo na amani ya nchi yetu tuendelee kudumisha” DAS Peter Masindi.

Maadhimisho haya yanaambatana na uzinduzi wa dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025-2050 ,Kauli mbiu ya uhuru Mwaka 2023 ni "Miaka 62 ya Uhuru umoja na mshikamano ni chachu ya Maendeleo ya Taifa letu


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.